· Disemba, 2009

Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Disemba, 2009

Podikasti: Mahojiano na Sudanese Drima

Sudanese Drima ni jina la bandia la mwandishi wa Kisudani wa Global Voices anayeishi nchini Malaysia. Katika mahojiano haya ya dakika kumi tunajadili jinsi uanahabari wa kijamii unavyoathiri Uislamu, mgogoro wa dafur, na masuala ya nafsi ya Uafrika-Uarabu katika Asia ya Kusini Mashariki.

Singapore: Kampeni ya “Kataa Ubakaji”

  23 Disemba 2009

Nchini Singapore, mara nyingi kumbaka mke wako hakuchukuliwi kama tendo la kubaka. Waandaji wa kampeni ya “Kataa Ubakaji” wanataka kukomesha sheria inayokinga ubakaji ndani ya ndoa kwa kuzindua kampeni ya kukusanya saini ambazo zitawasilishwa kwa watunga sera. Wengi wa raia wa mtandaoni wanaiunga mkono kampeni hii.

Misitu ya Madagascar Inateketezwa kwa $460,000 kwa Siku

Wakati mataifa ya dunia yanakutana huko Copenhagen kwa ajili ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi, Madagascar, ambayo imekwishapoteza 90% ya misitu yake ya asili, inakabiliwa na tishio la biashara ya magendo ya magogo, inayotishia kuharibu kile kilichobakia katika moja ya mifumo ya mazingira yenye viumbe na mimea mingi inayotofautiana.

Morocco: Mwanablogu Mwingine Atupwa Gerezani

  20 Disemba 2009

Mnamo tarehe 14 Desemba, siku ya Jumatatu, mwanablogu Bashir Hazzam na mmiliki wa mgahawa wa Intaneti Abdullah Boukhou walihukumiwa kifungo cha miezi minne jela kwa huyo wa kwanza na mwaka mmoja kwa huyo wa pili pamoja na kulipa faini ya MAD 500 (sawa na dola za Marekani 63) kila mmoja katika mahakama ya Goulmim.

Brazil: Wito wa Kugomea Gazeti Linaloongoza Nchini

  14 Disemba 2009

Wanablogu wa Brazili wamekuwa wakihamasisha mgomo dhidi ya kile walichokiita Coupist Press Party, yaani Sherehe ya Chombo cha Habari ya Kutaka Kupindua Serikali, kwa hiyo wamekuwa wakiwataka watu kuacha kununua, kusoma au kutoa maoni na badala yake kufuta usajili wao kutoka kwenye gazeti la Folha de São Paulo na tovuti yake.