Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Oktoba, 2008
Chile: Mkutano wa McCain na Pinochet Mwaka 1985
Mwaka 1985, Mbunge wa bunge la Marekani aitwaye John Mccain alizuru nchini Chile na kukutana na mtawala wa kiimla Augusto Pinochet, akiwa na viongozi wengine wa serikali. Mkutano huo ambao haujawahi kuripotiwa hapo awali umewekwa wazi na mwandishi wa habari John Dinges, ambaye amechapisha habari hiyo kwenye blogu yake CIPHER [es], kadhalika katika blogu ya Huffington Post, ambako huwa anaandika masuala yanayomhusu John McCain "ambaye amekuwa akishutumu vikali dhana ya kuketi na watawala wa kiimla bila ya masharti yoyote, inaonekana kuwa alifanya jambo hilo hilo analolipinga.
Misri: Sisi sote ni Laila
Sisi sote ni Laila, ndivyo wanavyosikika kusema kwa sauti moja wanablogu wa kike wa Misri. Hivi, huyu Laila ni nani na kwa nini wasichana na wanawake wa kiMisri wanapenda kufananishwa naye? Hebu endelea kusoma ili uone ni kwa namna gani wanablogu wa Misri wanavyojihangaisha ili kuvunjilia mbali vikwazo vya jinsia na kufanya sauti zao zisikike.
Afrika ya Kusini: VVU na UKIMWI na mabadiliko ya sera
Mwishoni mwa mwezi Septemba, Barbara Hogan, aliteuliwa na Rais wa mpito Kgalema Motlanthe kuwa waziri mpya wa afya wa Afrika ya Kusini, akichukua nafasi ya mtangulizi wake mwenye utata mwingi, Manto Tshabalala-Msimang. Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI na raia wengi wa Afrika ya Kusini wana matumaini makubwa kwamba hatua hii...
Marekani ya Kusini:Taarifa,Twita kwa Waandishi wa Habari Yapata Umaarufu
"Reporting On" ni zana mpya ya kublogu kwa kifupi na inachukua umaarufu mkubwa katika kundi la wanahabari wa Marekani ya Kusini (Walatino) ambao wanatumia zana hii ili kupashana habari na wengine kuhusu yale wanayoyaandika.
Afrika Ya Kusini: Mjomba, Urais Uko Wapi?
Ulimwengu wa blogu nchini Afrika ya Kusini umelipuka kutokana habari za hivi karibuni kuhusu mawaziri 11 na manaibu 3 kujiuzulu wakiwemo mawaziri vinara, Trevor Manuel na Naibu Rais, Phumzile Mlambo-Ngcuka. Yafuatayo ni yale wanayosema mabloga …