Habari kuhusu Habari Kuu kutoka Aprili, 2011
Kenya: Uanahabari wa kiraia wa Mtandao wa Habari wa Kibera
Vijana wa Kibera, Kenya, kitongoji ambacho kinajulikana kwa baadhi kama eneo kubwa la hovyo zaidi ya yote barani Afrika, wamedhamiria kuonesha sura nyingine ya mahali wanapoishi. Huku wakiwa na kamera mkononi, wanavinjari mitaa kutafuta habari kuinesha dunia jinsi Kibera inavyojiona yenyewe.
Misri: Mubarak awekwa Kizuizini
Miezi michache tu iliyopita, raia wengi wa Misri walitamani sana kumwona aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Rais Mubarak, akitupwa jela, hata hivyo, pengine ni wachache miongoni mwao waliofikiri kwa uhakika kabisa kwamba siku moja jambo hili lingetimia. Hata hivyo, mnamo Jumatano ya tarehe 13 Aprili, 2011, raia wa Misri waliamka na mapema asubuhi ya siku hiyohiyo kukutana na habari zinazohusu Mubaraka kutupwa kizuizini. Hapa chini tunawaletea jinsi habari hizi zilivyopokelewa katika ulimwengu wa uandishi wa habari wa Kijmii miongoni mwa Wamisri.
Attahiru Jega: Kiongozi wa Tume ya Uchaguzi ya Naijeria au Mtekaji?
Watumiaji wa mtandao wa Intaneti wa Naijeria wanadai kwamba utando usio na mwangaza wa siasa za Naijeria unahitaji mwamuzi mwenye uwezo wakati wa Uchaguzi wa 2011. Attahiru Jega, bosi wa tume ya uchaguzi itabidi adhihirishe katika majuma yajayo kuwa uchaguzi utakuwa mwepesi kama A, B, C.
Côte d'Ivoire: Kuanguka kwa Laurent Gbagbo
Laurent Gbagbo alikamatwa katika makazi yake ya Cocody, pamoja na mkewe, Simone, na msafara wa watu wa karibu. Miezi mitano baada ya kukataa kukabidhi madaraka kwa rais anayetambuliwa kimataifa kama rais mpya wa Côte d'Ivoire, Alassane Ouattara, mgogoro nchini humo hivi sasa unaelekea kufikia hitimisho.Mtiririko wa matukio yaliyopelekea kukamatwa kwa Gbagbo yaliorodheshwa kwa kina kwa njia ya video za kwenye mtandao ambazo zilitolewa maoni kwenye mtandao.
Côte d'Ivoire: Gbagbo agoma, Waafrika waandamana
Wakati Rais wa zamani wa Côte d'Ivoire Rais Laurent Gbagbo akiwa bado amejichimbia ndani ya handaki nchini humo, akigoma kukamatwa kwa kuendelea kukataa kushindwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2010, ushiriki wa Ufaransa katika harakati za kumng’oa zinasababisha miitikio miongoni mwa wanasiasa na raia wa Ufaransa, pamoja na jamii ya Waafrika waishio Ufaransa.
Côte d'Ivoire: Abijani kwenye masaa ya kudhoofu kwa utawala wa Gbagbo
Siku mbili zilizopita zimekuwa na utajiri katika misuguano na mivutano nchini Côte d'Ivoire. Vikosi vinavyomtii Ouattara, vilianza mashambulizi kuelekea Kusini na Magharibi mwa nchi hiyo. Katika siku zisizozidi tatu, walifanikiwa kuikamata miji ya Douékoué na kufika Yamoussoukro tarehe 30 Machi. Wa-Ivory wanatoa maoni yao kuhusu wafungwa kutoroka, kufungwa kwa televisheni ya taifa na sehemu aliyo Gbagbo:
Naijeria: Je, Teknolojia itaathiri uchaguzi wa mwaka 2011?
Wanaijeria wanaingia kwenye uchaguzi tarehe 16 Aprili 2011 kumchagua rais wao mpya. Uchaguzi uliahirishwa kutoka siku iliyokuwa imepangwa awali ya Aprili 9 kwa sababu ya kasoro za kimuundo. Katika makala hii tunatazama namna Wanaijeria wanavyotumia teknolojia kuwezesha uwazi katika uchaguzi, ushirikishwaji wa kisiasa na utawala bora.
Ivory Coast: Je, nani anadhibiti televisheni ya taifa ya RTI?
Bado kuna mkanganyiko kuhusu swali la nani hivi sasa ndiye mwenye udhibiti wa Radio Télévision Ivoirienne (RTI) , ambacho ni kituo cha televisheni ya taifa.
Myanmar: Simulizi za Wafanyakazi wa Misaada Baada ya Tetemeko la Ardhi
Myanmar bado inasumbuka kutokana na tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.8 ambalo liliikumba nchi hiyo. Mwandishi wetu aliyeko Myanmar anatafsiri mahojiano na simulizi za wakazi pamoja na wafanyakazi wa misaada ambao walishuhudia kiwango cha uharibifu uliofanywa na tetemeko hilo kaskazini mashariki mwa Myanmar.
Japan: Jijini Tokyo baada ya Tetemeko la Ardhi
Makala hii ni sehemu ya habari maalumu za Tetemeko la Japani 2011. Siku ya Ijumaa, Machi 11, 2011 saa 8:46:23 mchana kwa saa za Japani, , tetemeko lenye kipimo cha 8.9 liliikumba Japan, hili ni tetemeko kuwahi kutokea katika historia iliyorekodiwa. (Wakati makala hii inaandikwa kwa mara ya kwanza ilikuwa)...