Habari kuhusu Moroko

Morocco: Wanafunzi Wadai Marekebisho kwenye Mfumo wa Elimu

  18 Agosti 2012

Mwezi Julai, kikundi cha wanafunzi wa nchini Morocco kilizindua ukurasa wa Facebook ulioitwa "Umoja wa Wanafunzi wa Morocco kwa ajili ya Mabadiliko ya Mfumo wa Elimu". Pungufu ya mwezi mmoja, kikundi hiki kilivuta uungwaji mkono mkubwa hasa kupitia mitandao ya kijamii.

Moroko: Mtoto Mwanablogu Asalimia Ulimwengu

  16 Agosti 2010

Salma alianza kublogu akiwa na umri wa miaka sita ili kuwasiliana na ndugu na marafiki. Chii ya usimamizi wa wazazi wake, mwanablogu huyu mdogo wa Moroko anapendelea kuandika hadithi fupi fupi na kuielezea dunia matukio anayokumbana nayo kila siku shuleni.

Moroko: Je, Wakristu Wako Hatarini?

  9 Aprili 2010

Mapema mwezi Machi mwaka huu, watazamaji walishuhudia jumla ya wafanyakazi wa muda mrefu katika kituo cha Kikristo cha kulelea watoto yatima wapatao 20 wakifukuzwa kutoka katika nchi ambayo wanaiona kama nyumbani. Tukio hilo pamoja na mengine kadhaa yaliyofuatia yamezusha mjadala kuhusiana na imani ya Kikristu katika ufalme huo.

Morocco: Kusherehekea Idi katika Sehemu za Mashambani

  13 Disemba 2009

Wikiendi hii iliyopita, Wamoroko walisherehekea Eid Al-Adha. Wanablogu walioko sehemu za vijijini nchini Moroko wanasimulia simulizi zao kuhusu Eid ya mwaka huu. Kwa kuwa upatikanaji wa intaneti upo sehemu chache n amara nyingi ni wa aghali mno nje miji mikubwa, wengi wanaoblugu kutokea sehemu za mashamba ni Wafanyakazi wa Amani wa Kujitolea (PCVs) na kwa hiyo wako katika nafasi ya kuweza kutoa mitazamo kama wageni kutoka nje… walioko ndani.

Twita Kutoka Beirut: Siku ya Pili ya Warsha ya Wanablogu wa Uarabuni

  12 Disemba 2009

Siku ya pili ya Warsha ya Wanablogu wa Kiarabu ilianza na mada inayohusu Mtandao wa Herdict, tovuti inayotumia vyanzo vya watumiaji kukusanya taarifa za uchujaji wa habari kwenye intaneti kutoka kwa watumiaji duniani kote. Mshiriki wa warsha kutoka Qatar Muhammad Basheer alituma picha kutoka kwenye mada hiyo katika ujumbe wa...

MENA: Maoni Wakati Wa Kuapishwa Obama

  26 Januari 2009

Tukio la kihistoria limetokea Marekani leo wakati Barack Obama alipoapishwa kuwa rais wa 44. Wakati kuungwa mkono kwa Obama kati ya Waarabu kumekuwa kukipungua katika miezi michache iliyopita kufuatia uteuzi wake wa baraza la mawaziri na ukimya wake kuhusu mashambulio ya Israeli huko Gaza, wanablogu wa Mashariki ya Kati na...