10 Julai 2013

Habari kutoka 10 Julai 2013

Saudi Arabia: Familia za Wanaoshikiliwa Gerezani Zaandamana

Familia za watu wa Saudi Arabia wanaoshikiliwa gerezani yaingia siku ya tatu ya kupinga kushikiliwa kwa wapendwa wao bila sababu maalum. Saudi Arabia ni moja ya nchi chache duniani ambazo bado zipo chini ya mfumo wa utawala wa kifalme na ina rekodi isiyoridhisha kuhusu haki za binadamu ikiwa ni pamoja na kushikilia gerezani zaidi ya watu 30,000 bila sababu maalum.

Global Voices Yazindua Ushirikiano na Shirika la NACLA

Global Voices na Shirika la Marekani Kaskazini Linaloshughulika na Amerika Kusini (NACLA) wameanzisha ushirikiano mpya ambao utaleta kwa pamoja dira ya Sauti za Dunia ya habari za kiraia na na ile ya NACLA ya uchunguzi na utoaji wa elimu, lengo likiwa ni kuwaletea wasomaji wetu habari halisi na za kina kutoka katika eneo hili la Latini Amerika.