· Disemba, 2009

Habari kuhusu Vyombo na Uandishi wa Habari kutoka Disemba, 2009

Tunisia: Mwanafunzi Atupwa Gerezani kwa Kuhojiwa na Chombo cha Habari

Wanaharakati nchini Tunisia wamezindua ukurasa wa Facebook na blogu ili kumuunga mkono Mohamed Soudani, 24, aliyetoweka mnamo tarehe 22 Oktoba 2009 nchini humo mara baada ya kufanya mahojiano na Redio Monte Carlo International na vilevile Redio France International. Tangia hapo marafiki walipata fununu kwamba alikamatwa na kutupwa korokoroni na kuteswa vibaya.

15 Disemba 2009

Brazil: Wito wa Kugomea Gazeti Linaloongoza Nchini

Wanablogu wa Brazili wamekuwa wakihamasisha mgomo dhidi ya kile walichokiita Coupist Press Party, yaani Sherehe ya Chombo cha Habari ya Kutaka Kupindua Serikali, kwa hiyo wamekuwa wakiwataka watu kuacha kununua, kusoma au kutoa maoni na badala yake kufuta usajili wao kutoka kwenye gazeti la Folha de São Paulo na tovuti yake.

14 Disemba 2009

Urusi: Jinsi Abiria wa “Nevsky Express” Walivyoeleza Habari Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Kijamii

Ajali ya treni la "Nevsky Express" ilitokea mbali na makazi ya watu. Ilichukua masaa kadhaa kwa wanahabari kufika kwenye eneo. Na hapo ndio picha na video za kwanza zilipoanza kuonekana kila mahali. je nini kilichotokea kwenye upashanaji habari wa kiraia ambao uliongoza njia ya kupashana habari wakati wa ajali ya ndege huko Urusi mwaka mmoja uliopita?

1 Disemba 2009