Habari kutoka 30 Mei 2013
Lebanon: Mwanablogu Apata Kipigo kwa Kupiga Picha
Mwanablogu wa ki-Lebanoni Habib Battah anaeleza namna alivyoshikiliwa bila hiari, akilazimishwa kufuta picha katika kamera ya simu yake na kudhalilishwa mfululizo katika posti hii inayohusiana na ripoti ya Beirut. Aliporipoti suala hilo katika kituo cha polisi mahali alipokuwa, mafisa wanaohusika walimkana na kumgeuzia kibao yeye. Anaongeza: Walikuwa sahihi. Kama watu...
Wafanyakazi Wavamia Majengo ya Serikali Nchini Mauritania
Siku ya Jumanne asubuhi, Mei 28, 2013, maelfu ya vibarua, wanaolipwa ujira wao kwa kufanya kazi kwa siku, walianzisha maandamano makubwa [ar] huko Zouérat, mji mkuu wa jimbo la Tiris Zemmour kasikazini mwa Mauritania, wakidai mikataba inayoeleweka na haki zao nyinginezo ikiwa ni pamoja na kumalizwa kwa ukiritimba wa wafanyabiashara...
Mwandishi Habari za Kiraia wa Miaka 14 Auawa Akiripoti Mapigano Nchini Syria
Omar Qatifaan, mwanaharakati wa Habari mwenye umri wa miaka 14 ameuawa akiwa katika jitihada za kutangaza habari za mapigano kati ya vikosi vya kijeshi vinavyoiunga mkono serikali na vile vya waasi katika eneo la Daraa al-Ballad kusini mwa Sryria karibu na mpaka wa Jordan.