Habari kutoka 24 Oktoba 2009
Trinidad & Tobago: Mtrini Mpaka Kwenye Mifupa?
“Kila siku ambayo ninapitia habari ninazidi kushawishika kuwa ninataka kuachana na klabu ya ‘Mimi ni Mtrini’ na kwenda sehemu nyingine”: Coffeewallah ameshachoka na kila kitu kuanzia uhalifu mpaka kodi.
Uanaharakati na Umama Barani Asia
Je, mwanamke anatoa sadaka zipi ili kupigania jambo analiamini? Je, watoto wake wanaathiriwa vipi na mateso yanayoelekezwa kwake? Makala hii inachambua kwa kifupi maisha ya wanawake wanaharakati katika Asia ambao pia ni ma-mama.
Uganda: Wanablogu wa Uganda Wajadili Muswada Unaopinga Ushoga
Muswada ambao utaufanya ushoga kuwa kingyume cha sheria nchini Uganda umewasilishwa bungeni na sasa unasubiri tu saini ya rais Yoweri Museveni. Wanablogu mashoga nchini uganda wanajadili.
China: Maisha ya Raia wa Kigeni Katika Jela ya Beijing
Raia wa kigeni ambaye alitumia muda wa miezi saba iliyopita katika jela ya Beijing No. 1 Detention Center aliitumia idhaa ya DANWEI maelezo ya kina ya maisha yake ya kila siku katika jela hiyo.
China: Ndoto ya Nobel
Kila mwaka, wakati wa kutangaza mshindi wa Tuzo ya Nobel unapowadia, Wachina hugubikwa na hamasa fulani hivi. Endapo mshindi ni yule wa asili ya Uchina, basi wao hufurahi sana. Lakini mara baada ya kupita siku chache, furaha hiyo huanza kupoa au hata kugeuka na kuwa simanzi. Mwaka unaofuata wakati unapowadia tena, hali hujirudia tena kama hapo awali.