makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Juni, 2012
Sudani: Kuondoa kizuizi cha Mapinduzi ya Sudani
Tofauti na nchi nyingine katika eneo lake, Sudani mara nyingi huwa haipati nafasi katika vyombo vikuu vya habari, na hili lilikuwa wazi zaidi wakati wa maandamano yalifanyika Ijumaa na Jumamosi. Sababu ni kwamba serikali ya Sudani imevibana mno vyombo vya ndani vya habari na kuwazuia waandishi kuripoti habari zinazohusu masuala ya haki za binadamu na ufisadi.
Sudani: “Polisi Yakanusha Kutumia Risasi; Majeruhi wote ni Wakufikirika
Maafisa wa serikali ya sudani wanarudia ‘uongo’ uliozoeleka ambao watawala wa ki-Arabu wamekuwa wakitumia tangu kuanza kwa yale yanayoitwa Mapinduzi ya Uarabuni yaliyoanza mwezi Desemba 2010. Imekuwa kawaida kusikia kauli kama, ‘waandamanaji wamedhibitiwa wakati wakiwashambulia polisi, ambao nao walijihami kwa kushambulia' Watumiaji wa mtandao wanaonyesha picha tofauti wakati tetesi zinadai mtandao wa intaneti utakatwa kufuatia kuongezeka kwa maandamano.
Sudani: Watumia Mtandao Wathibitisha Tetesi za Kukatwa kwa Intaneti
Raia wa kwenye mtandao wanaifuatilia kwa karibu Sudani, kufuatia tetesi kuwa serikali ya Sudani inadhamiria kuukata mtandao wa intaneti - hatua inayokumbushia jaribio la Misri kuwanyamazisha wanaharakati na kuthibiti mapinduzi ya Januari 25 pale ilipoondoa uwezekano wa watu kuwasiliana kwa mtandao wa intanenti mnamo Januari 27.
Kenya: Kilimo cha Bustani Mijini Chashika Kasi
Nchini Kenya, wakazi wa mjijini wanajifunza mbinu mbalimbali za kulima mazao ya chakula kwa ajili ya matumizi binafzi na kwa ajili ya kuuza katika maeneo madogo. kwa watu wenye kipato kidogo au wasio na kipato, ukulima wa mijini unaweza kuwa ndiyo ufumbuzi wa kujihakikishia uwepo wa chakula. Video hizi zinaonyesha jinsi ambavyo chakula kinaweza kuzalishwa katika makasha na vifaa vingine vya kubebea kwa kutumia maeneo na rasilimali kidogo.
Mabadiliko ya Mfumo wa Ustawi wa Jamii ya Kiafrika
Utekelezaji wa mifumo ya hifadhi ya jamii ya taifa bado uko katika hatua za mabadiliko katika nchi nyingi za Afrika. Mafanikio ya mifumo iliyopo yanajadiliwa na wataalamu wa hifadhi za jamii katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara.
Ethiopia: Ardhi, Historia na Haki katika Eneo la Gambella
Wanaharakati wa masuala ya ardhi wanatumia hati ya malalamiko ya mtandao, mtandao wa facebook na twita kufanya kampeni dhidi ya unyang’anyi wa ardhi nchini Ethiopia. Inaarifiwa kwamba wanakijiji kwenye jimbo msikini zaidi nchini humo, Gambella, wanalazimishwa kuhamia kwenye vijiji vilivyobuniwa na serikali ili kuwapisha wanaoitwa 'wawekezaji' wakubwa.
Misri: Maandamano ya Kukomesha Udhalilishaji wa Kijinsia Yavamiwa
Maandamano kudai kukomeshwa kwa udhalilishaji wa kijinsia yaligeuka kuwa shubiri baada ya wanawake waliokuwa wanahusika nayo kuvamiwa na kundi la wanaume wenye hasira kwenye viwanja vya Tahrir leo(June 8, 2012). Watu walioshuhudia tukio hilo walielezea maoni yao kupitia twita.
Zambia Yapanga Bei ya Mahindi kwa Mara Nyingine, Yaikasirisha Benki ya Dunia
Kupanda kwa bei ya mahindi, chakula kikuu nchini Zambia kumesababisha raia kufanya ghasia na hata kusababisha jeshi kuingilia kati. Pamoja na tahadhari iliyotolewa na benki ya dunia kwamba hatua hiyo ingeathiri sekta ya kilimo, watawala wa nchi hiyo wameendelea kupanga bei ya unga wa mahindi.
Uganda: Je, Uganda inageuka kuwa dola ya kifalme?
Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni amekuwa madarakani tangu mwaka 1986. Majuma machache yaliyopita, wananchi walianza kudodosa habari za nani hasa atamrithi kama ataamua kutokugombea kwa awamu ya nne mwaka 2016. Tetesi zinadai kwamba rais anamwunga mkono mkewe, Waziri wa mambo ya Karamoja kurithi kiti cha rais.
Kenya: Habari za Mlipuko Jijini Nairobi Zatawala Mijadala ya Twita
Kufuatia mlipuko mkubwa ulioathiri vibaya mtaa mkubwa wa Nairobi, Moi Avenue, wakenya na marafiki wa Kenya walitumia mtandao wa twita kuhabarishana, na kusambaza taarifa, kushauriana na kujadili tukio hilo baya.