Mghosya · Julai, 2012

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Julai, 2012

Tanzania: Mgomo wa Walimu Watikisa Nchi

Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kufanyika zoezi la sensa, walimu nchini Tanzania wako katika mgomo kuishinikiza serikali kuwalipa madai yao pamoja na kuboresha mishahara yao. Hatua hiyo imevuta hisia za watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii wanaojadili madhara ya mgomo huo.

31 Julai 2012

Cameroon: Ndoto za Umeme kwa Ajili ya Maendeleo ifikapo 2035

Cameroon inatarajiwa kufikia hadhi ya soko linalokua kwa kasi ifikapo mwaka 2035 kupitia "mafanikio makubwa" ya hatua kwa hatua katika maendeleo ya miundombinu ya usafiri na nishati. Hata hivyo kufikiwa kwa malengo hayo ndani ya muda uliopangwa hakuonekani kuwashawishi wachambuzi wengi wa masuala ya kisiasa, kwa sababu tu changamoto zilziopo ni nyingi.

8 Julai 2012

Misri: Mubarak Afariki Dunia kwa Mara Nyingine

Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak amewahi kufa angalau mara moja kwa kila baada ya majuma machache tangu kuanza kwa mapinduzi ya Misri, yaliyouangusha utawala wake uliodumu kwa miaka 32. Watumiaji wa mtandao wanaitikia tetesi za hivi karibuni kuhusu afya yake.

7 Julai 2012

Cuba: Maandamano yafanyika Mara Mbili, Wengi Wakamatwa

Kikundi cha wanawake kijiitacho ‘wanawake wavaliao mavazi meupe’ (Ladies in White) kwa mara nyingine wametawala fikra za wanablogu wa Cuba waishio nje ya nchi. Maandamano ya amani ya kikundi hicho ambacho ni moja wapo ya vyombo vya upinzani vinavyoheshimika zaidi katika visiwa hivyo –pamoja na kukamatwa kwao mara kwa mara na vyombo vya dola –yanaendelea kuvuta hisia za watu. Mapambano ya hivi karibuni yalitokea mwishoni mwa juma lililopita wakati wanachama wa kikundi hicho walipojaribu kufanya maandamano mara mbili mjini Havana.

7 Julai 2012

Tazama Picha za Afghanistan Ambazo Huwa Huzioni

Vyombo vingi vya habari vinavyovipoti hali inavyoendelea nchini Afghanistan hubeba taswira mbya. Kupitia miwani yao, Afghanistan huoneshwa kama nchi inayozama kwenye vimbi la mapigano na sura ya kijeshi. Wapiga kura kadhaa wanawasaidia watu kuona nchi hiyo iliyoathiriwa na vita lakini nzuri kwa mtazamo tofauti.

7 Julai 2012