Mghosya · Oktoba, 2009

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Oktoba, 2009

Malayasia: Serikali ya Jimbo Yaja na Sera ya ‘Msala Mmoja’

Kwa kuiga chapa ya Malaysia1, serikali ya Jimbo la Terengganu hivi majuzi ilikuja na sera ya ‘msala 1’ kama hatua kwa walimu na wanafunzi (wa jinsia moja) kuchangia misala (vyoo) ili kukuza hisia za umoja. Kumekuwepo na maoni mchanganyiko katika ulimwengu wa blogu kuhusiana na sera hii.

27 Oktoba 2009

Marekani: Wanandoa wa rangi tofauti wanyimwa cheti cha ndoa

Juma lililopita huko Hammond, Louisiana, wapenzi wawili walituma maombi ya kibali cha kufunga ndoa na walikataliwa kwa misingi ya rangi zao tofauti. Afisa wa kutathmini na kuandikisha nyaraka (Muamuzi wa Amani) alidai kuwa “ndoa baina ya watu wa rangi hazidumu” na alisema kuwa anafanya hivyo “kwa ajili ya watoto.”

25 Oktoba 2009

Ghana: Siku ya Kublogu mwaka 2009

Kwenye siku ya Kublogu Kwa Vitendo Duniani, Waghana waliwahoji viongozi wa dunia, walichachafya karatasi za Benki ya Dunia, walitambulisha tovuti mpya na walijiuliza ni kwa nini kulikuwa na majadiliano machache sana yanayohusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa nchini – na pia walitambua kwamba kuna mambo fulani nchi kama Ghana zinayafanya vyema.

23 Oktoba 2009

Big Brother Africa msimu wa IV: Mageuzi yameanza

Big Brother Africa 4: Mapinduzi ni mfululizo wa nne wa vipindi vya kituo cha televisheni vinavyoonyesha maisha halisi vya Big Brother Africa, vilivyoanza Septemba 6, 2009. Kipindi hicho kimeshaanza kuzua mijadala na maoni kwenye mtandao wa intaneti kutoka kwa wanablogu na wasomaji wao.

17 Oktoba 2009

Gabon: Upinzani waendelea kupinga matokeo ya Uchaguzi

Wapinzani wa kisiasa wa Gabon wanaonyesha muungano wa vyama vya siasa kupinga matokeo ya uchaguzi wa mwezi Agosti, ambayo yalimkabidhi urais mwana wa mtawala wa kiimla aliyepita, Omar Bongo. Wanasiasa na raia wanaikemea Ufaransa kwa kuingilia siasa za nchi hiyo.

12 Oktoba 2009