Mghosya · Mei, 2013

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Mei, 2013

Ijue Mauritania kwa Jicho la Msanii wa Kireno

Msanii wa Kireno Isabel Fiadeiro anayeishi katika mji wa Nouakchott, Mauritania, ambako anachora na kuendesha maonyesho ya kazi ya sanaa. Fiadeiro vilevile huchora madhari kwa kuyatazama, hujaza blogu yake anayoiita Michoro nchini Mauritania na michoro ya maisha ya kila siku katika taifa hilo la Afrika Magharibi. Global Voices ilizungumza na Fiadeiro kuhusu kazi yake ya sanaa na namna michoro yake ilivyomsaidia kuifahamu Mauritania.

31 Mei 2013

Saudi Arabia Yawanyonga Raia Watano wa Yemeni na Kutundika Miili Yao Hadharani

Raia watano wa Yemeni waliotiwa hatiani kwa mauaji na ujambazi walinyongwa kwa kukatwa kichwa nchini Saudi Arabia na miili yake kuanikwa hadharani huko Jizan, mji ullio kusinimagharibi mwa nchi hiyo. Picha za miili hiyo ikining'inia kwenye kamba hewani ilisambaa kwenye mtandao wa Twita na facebook kama hatua ya wa-Yemeni kupinga ukatili huo.

26 Mei 2013