makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Mei, 2013
Ijue Mauritania kwa Jicho la Msanii wa Kireno
Msanii wa Kireno Isabel Fiadeiro anayeishi katika mji wa Nouakchott, Mauritania, ambako anachora na kuendesha maonyesho ya kazi ya sanaa. Fiadeiro vilevile huchora madhari kwa kuyatazama, hujaza blogu yake anayoiita Michoro nchini Mauritania na michoro ya maisha ya kila siku katika taifa hilo la Afrika Magharibi. Global Voices ilizungumza na Fiadeiro kuhusu kazi yake ya sanaa na namna michoro yake ilivyomsaidia kuifahamu Mauritania.
VIDEO: Namna Watu Wawili Tofauti Walivyopinga Dhuluma na Kushinda
Mkhuseli "Khusta" Jack na Oscar Olivera waliongoza harakati tofauti za kiraia zisizohusisha vurugu, moja ikiwa ni Afrika Kusini mwaka 1985 nyingine ikiwa ni Bolvia mwaka 2000. Video iliyoandaliwa na Shule ya Uandishi wa Weledi inasimulia habari zao
Lebanon: Mwanablogu Apata Kipigo kwa Kupiga Picha
Mwanablogu wa ki-Lebanoni Habib Battah anaeleza namna alivyoshikiliwa bila hiari, akilazimishwa kufuta picha katika kamera ya simu yake na kudhalilishwa mfululizo katika posti hii inayohusiana na ripoti ya Beirut. Aliporipoti...
Wafanyakazi Wavamia Majengo ya Serikali Nchini Mauritania
Siku ya Jumanne asubuhi, Mei 28, 2013, maelfu ya vibarua, wanaolipwa ujira wao kwa kufanya kazi kwa siku, walianzisha maandamano makubwa [ar] huko Zouérat, mji mkuu wa jimbo la Tiris...
Kwa nini Mashirika ya Umma Yameshindwa Nchini Zambia
Elias Munshya, mwanasheria na mchungaji wa Zambia, anaeleza kwa nini mashirika ya umma yamedumaa nchini Zambia tangu uhuru: Mashirika ya umma hayajawahi kutengeneza faida tangu mwaka 1964. Yamekuwa yakiendeshwa kiholela...
Botswana: Kuibwa kwa Kazi ya Sanaa ya “Bushman's Secrets”
MyWeku anaichambua filamu yenye maudhui halisi (documentary) inayoelezea wizi wa kazi ya sanaa ya Sana iitwayo “Bushman's secrets”: Filamu hii inachora picha inayosikitisha ya namna ambavyo Uniliver, kampuni inayojinadi kama...
Rais wa Chama cha Madaktari Msumbiji Akamatwa
Baada ya mgomo wa madaktari uliodumu kwa takribani juma moja nchini Msumbuji, Dr. Jorge Arroz, Rais wa Associação Médica de Moçambique, amekamatwa usiku wa Jumapili, Mei 26, 2013, kwa tuhuma...
Saudi Arabia Yawanyonga Raia Watano wa Yemeni na Kutundika Miili Yao Hadharani
Raia watano wa Yemeni waliotiwa hatiani kwa mauaji na ujambazi walinyongwa kwa kukatwa kichwa nchini Saudi Arabia na miili yake kuanikwa hadharani huko Jizan, mji ullio kusinimagharibi mwa nchi hiyo. Picha za miili hiyo ikining'inia kwenye kamba hewani ilisambaa kwenye mtandao wa Twita na facebook kama hatua ya wa-Yemeni kupinga ukatili huo.
Rafael Correa Aapishwa kwa Kipindi cha Tatu Kama Rais wa Ekuado
Rafael Correa ameapishwa kuingia ikulu kama Rais wa Jamhuri ya Ekuado kutawala mpaka 2017..
Shambulio la Mabomu Mawili ya Kujitoa Muhanga Nchini Niger Yaua Watu 23
Benjamin Roger wa Jeune Afrique anaripoti [fr] kuwa wanajeshi 18, raia mmoja na magaidi wanne waliuawa mapema subuhi ya leo katika shambulio la mabomu ya kujitoa Muhanga kwenye gari mjini...