makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Aprili, 2011
Misri: Basboussa kwa Urais!
Mtangazaji habari wa zamani wa televisheni ya Misri na mwanaharakati Bothaina Kamel alitangaza kwenye twita kwamba ana mipango ya kugombea urais. Yafuatayo ni maoni ya kumuunga mkono na kupinga hiyo mipango yake .
Naijeria: Wafuatiliaji wa twita unaoweza kuwafuatilia wakati wa Uchaguzi wa Naijeria mwaka 2011
Ni wakati wa uchaguzi nchini Naijeria. Uchaguzi wa Wabunge umeahirishwa mpaka Jumatatu kutokana na hitilafu za kiuratibu. Uchaguzi wa Rais utafanyika tarehe 9 Aprili 2011. Hii ni orodha yetu ya kwanza ya watumiaji wa twita waliopendekezwa kama utapenda kufuatilia uchaguzi wa Naijeria 2011.
Naijeria: Wanablogu wa Ki-Naijeria wanasema nini kuhusu uchaguzi wa mwaka 2011?
Kadiri uchaguzi wa mwaka 2011 nchini Naijeria unavyozidi kukaribia, Wanablogu wa Naijeria wanatumia muda wao mwingi kuzungumza juu ya uchaguzi huo lakini je kuna mtu anayesikiliza?
Attahiru Jega: Kiongozi wa Tume ya Uchaguzi ya Naijeria au Mtekaji?
Watumiaji wa mtandao wa Intaneti wa Naijeria wanadai kwamba utando usio na mwangaza wa siasa za Naijeria unahitaji mwamuzi mwenye uwezo wakati wa Uchaguzi wa 2011. Attahiru Jega, bosi wa tume ya uchaguzi itabidi adhihirishe katika majuma yajayo kuwa uchaguzi utakuwa mwepesi kama A, B, C.
Côte d'Ivoire: Gbagbo agoma, Waafrika waandamana
Wakati Rais wa zamani wa Côte d'Ivoire Rais Laurent Gbagbo akiwa bado amejichimbia ndani ya handaki nchini humo, akigoma kukamatwa kwa kuendelea kukataa kushindwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2010, ushiriki wa Ufaransa katika harakati za kumng’oa zinasababisha miitikio miongoni mwa wanasiasa na raia wa Ufaransa, pamoja na jamii ya Waafrika waishio Ufaransa.
Côte d'Ivoire: Abijani kwenye masaa ya kudhoofu kwa utawala wa Gbagbo
Siku mbili zilizopita zimekuwa na utajiri katika misuguano na mivutano nchini Côte d'Ivoire. Vikosi vinavyomtii Ouattara, vilianza mashambulizi kuelekea Kusini na Magharibi mwa nchi hiyo. Katika siku zisizozidi tatu, walifanikiwa kuikamata miji ya Douékoué na kufika Yamoussoukro tarehe 30 Machi. Wa-Ivory wanatoa maoni yao kuhusu wafungwa kutoroka, kufungwa kwa televisheni ya taifa na sehemu aliyo Gbagbo:
Naijeria: Je, Teknolojia itaathiri uchaguzi wa mwaka 2011?
Wanaijeria wanaingia kwenye uchaguzi tarehe 16 Aprili 2011 kumchagua rais wao mpya. Uchaguzi uliahirishwa kutoka siku iliyokuwa imepangwa awali ya Aprili 9 kwa sababu ya kasoro za kimuundo. Katika makala hii tunatazama namna Wanaijeria wanavyotumia teknolojia kuwezesha uwazi katika uchaguzi, ushirikishwaji wa kisiasa na utawala bora.
Japani: Iambieni Dunia isaidie
Picha zilizotafutwa na kuwekwa kwenye twita zinaweza kuleta mambo ya kushangaza. Tafuta herufi hizi “宮城” (Miyagi) na picha chache zitatokea kutoka kwenye wilaya hiyo, moja ya maeneno yaliyoharibiwa sana nchini Japani baada ya tsunami. Nenda chini, na picha moja inaonekana, yenye rangi ya kahawia na bluu mpaka utakapoibofya…
Japani: Tsunami yaathiri eneo la pwani, yaacha kila kitu kimeharibiwa
Kufuatia tetemeko kubwa kuwahi kutokea nchini, Japani imekumbwa na tsumani mbaya zaidi iliyowahi kutokea. Watu wengi nchini kote wameganda kwenye luninga zao wakati vipande vya habari vinavyoonesha tsunami lenye urefu wa zaidi ya mita 7 kwenda juu likisomba magari na majengo.
Japan: Jijini Tokyo baada ya Tetemeko la Ardhi
Makala hii ni sehemu ya habari maalumu za Tetemeko la Japani 2011. Siku ya Ijumaa, Machi 11, 2011 saa 8:46:23 mchana kwa saa za Japani, , tetemeko lenye kipimo cha...