makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Disemba, 2009
Misri: Makao Makuu ya Kuzimu Duniani
Wanablogu na wanaharakati wengi wa Kimisri wamekuwa wakikamatwa na Usalama wa Taifa katika nyakati tafauti kwa sababu mbalimbali –za kweli au za bandia –Wa7da Masreya aliwahoji wanablogu mbalimbali na kuweka makala ya kina kuhusu mbinu za utesaji na hila za kisaikolojia ambazo wanablogu wale wamekuwa wakikumbana nazo kwenye makao makuu ya Usalama wa Taifa katika wilaya ya Jiji la Nasr.
Canada Imesema Nini? Upotoshaji wa Habari Kwenye Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi
Serikali ya Canada inasemekana imetoa tamko la jazba leo, ikikanusha upotoshaji wa habari zinazodaiwa kufanywa nayo kwa mujibu wa Jarida la Wall Street likidai kwamba Canada imebadili sera yake na itakuwa ikikubaliana na malengo ya kupunguza hewa ya ukaa.
Wapiga picha wa Kiafrika, waandishi na wasanii wapata sauti zao kwenye blogu
Kadri Waafrika wengi wanavyozidi kugundua nguvu ya kublogu kama zana ya kutoa maoni kwa kiwango cha dunia nzima, tarakimu ya wanablogu imeongezeka na pia maudhui yanayopewa kipaumbele. Kwa tarakimu hiyo ya kukua kwa blogu, wasanii wengi wa Kiafrika wamejiunga, na ongezeko kubwa likionekana kwenye blogu za mashairi kama ilivyo kwa upigaji picha unaochipukia na blogu za sanaa za maonyesho. Tunazipitia baadhi.
Iran: Maandano ya Siku ya Mwanafunzi kwenye YouTube
Maelfu ya waandamanaji hawakuujali utawala wa Kiislamu leo kwa kuandamana wakati wa siku ya mwanafunzi, wakiimba kaulimbiu dhidi ya Ali Khamenei, kiongozi wa Jamuhuri ya Kiislamu, na wakipinga sera ya mambo ya nje ya serikali.
Ghana: Rais Atta Mills Dhidi ya Chama Chake Mwenyewe?
Katika miezi michache kuelekea uchaguzi wa Rais Hohn Evans Atta Mills, wa-Ghana wengi, pamoja na wale walio nje ya nchi, waliohofu kwamba ushindi wa chama cha New Democratic Congress (NDC) ungeweza kugeuka kuwa utawala mwingine wa mwanzilishi wa chama hicho na mtawala wa zamani wa kijeshi, Rais Jerry John Rawlings.
Morocco: Kusherehekea Idi katika Sehemu za Mashambani
Wikiendi hii iliyopita, Wamoroko walisherehekea Eid Al-Adha. Wanablogu walioko sehemu za vijijini nchini Moroko wanasimulia simulizi zao kuhusu Eid ya mwaka huu. Kwa kuwa upatikanaji wa intaneti upo sehemu chache n amara nyingi ni wa aghali mno nje miji mikubwa, wengi wanaoblugu kutokea sehemu za mashamba ni Wafanyakazi wa Amani wa Kujitolea (PCVs) na kwa hiyo wako katika nafasi ya kuweza kutoa mitazamo kama wageni kutoka nje… walioko ndani.
Austria: Jinsi Nyenzo Za Habari Za Kijamii “Zinavyoviwashia Moto Vyuo Vikuu”
Je, ulijua kwamba katika wakati huu vyuo vikuu vingi kote Ulaya vinakaliwa na wanafunzi? Vuguvugu hili lote limeratibiwa kwa kutumia nyenzo za uanahabari wa kijamii katika mtandao.
Namibia: Nafasi ya Vyombo Vipya vya Habari kwa Uchaguzi wa 2009
Uchaguzi wa rais na bunge la taifa la Namibia ulifanyika tarehe 27 na 28 Novemba 2009. Vyama vya siasa na mashirika yasiyo ya kiserikali yalitumia nyenzo kadhaa za habari za kijamii kupiga kampeni, kufuatilia na kuripoti Uchaguzi.
Warsha ya Wanablogu wa Uarabuni: Tafakuri ya Twita kwa Siku ya Kwanza
Wakati siku ya kwanza ya Warsha ya Pili ya Mwaka ya Wanablogu wa Uarabuni ikifungwa, tutaangalia tafakuri za washiriki kwa siku nzima, kujua wamejifunza nini na namna wanavyojisikia. Siku ilianza...
Thailand: Waziri Mkuu wa Zamani Afariki Dunia
Samak Sundaravej — Gavana wa Zamani wa Bangkok, mwendeshaji wa kipindi cha mapishi, na Waziri Mkuu wa 25 wa Thailand amefariki dunia tarehe 24 Novemba. Soma maoni ya wanablogu na wanatwita wa Bangkok