· Februari, 2014

Habari kutoka Muhtasari wa Habari kutoka Februari, 2014

Sababu 10 Kwa nini Siafiki Shariah Nchini Pakistan

  25 Februari 2014

Mmoja wa msemaji wa Taliban alijitoa kwenye majadiliano ya hivi karibuni na serikali ya Pakistan na kudai kuwa ajenda ni pamoja na kuanzishwa kwa sharia kali. Mwanablogu wa Pakistan na Mwandishi wa Habari Beena Sarwar alipinga wazo hilo kupitia tamko aliloliweka katika mtandao wa Facebook lenye kichwa cha habari ‘sababu...

Sinagogi Pekee Lililobaki Myanmar

  25 Februari 2014

Lilijengwa miaka 120 iliyopita, Sinagogi la Musmeah Yeshua lililoko eneo la Yangon ni Sinagogi pekee la wayahudi lililoyobaki katika eneo linaloongozwa na waumini wa dini ya Kibudha waishio nchini Myanmar. Mbali na kuwa kivutio cha utalii, pia limetajwa kama jengo la urithi la mambo ya kale katika mji huo.

Rais Yanukovych wa Ukraine ang'olewa madarakani

  24 Februari 2014

Baada ya maandamano, vurugu na upinzani dhidi ya serikali uliosababisha vifo vya watu wapatao 100, Bunge la Ukraine hatimaye limepiga kura ya kumwondoa Rais Viktor Yanukovych kama hatua ya kujibu shinikizo la waandamanaji. Tayari Rais Yanukovych amenukuliwa akisema hana mpango wa kutoroka nchi. Soma zaidi kupitia kiungo hiki [en]

Upasuaji wa Kwanza wa Moyo Kongo Brazzaville

Mtandao wa kimataifa wa Afya La Chaîne de l’Espoir (Maana yake Kiungo cha Matumaini) unaripoti kuwa watoto saba wa ki-Kongo waliokuwa na hali mbaya wamenufaika na upasuaji wa moyo [fr] uliofanyika Februari 14 mjini Brazzaville, Kongo. Kwa msaada wa Msaidizi wa Kongo Shirika lenyewe, Prince Béni na Maya, wote wakisumbuliwa na...

Wavenezuela Waishio Mexico Wawambia Waandamanaji: “Hamko Pekeyenu”

  24 Februari 2014

Hali ya mambo nchini Venezuela yaendelea kuzorota, huku pakiwa na maandamano na mikusanyiko nchi nzima ayalisababisha vifo vya watu kumi na mamia kujeruhiwa mpaka sasa. Wavenezuela duniani kote wanaopinga serikali yao wameandaa mikusanyiko ya amani kupaza sauti zao na kuzifanya serikali za nchi wanazoishi kuelewa mwenendo wa mambo. Mexico haija...

Vyombo Vikuu vya Habari Vyaihujumu Facebook

  24 Februari 2014

Mwanablogu wa Teknolojia Amitha Amarasinghe anadai kwamba mtandao wa Facebook unapewa taswira hasi na vyombo vikuu vya habari nchini Sri Lanka kwa vichwa vya habari kama “Mwanafunzi ajiua shauri ya picha iliyowekwa Facebook”, “Mapenzi ya Facebook yaishia na kifo” na kadhalika. Ghafla tu, kuna mwongezeko mkubwa wa maudhui yanayotoa taswira...

Pongezi kwa Waziri Mkuu Mpya wa Nepal

  23 Februari 2014

Bunge la Nepal limemchagua Bw. Sushil Koirala (75), rais wa chama cha Nepali Congress, kuwa Waziri Mkuu wa Nepal. Mwanablogu wa NNepali aishiye ughaibuni Indra anampongeza Waziri Mkuu mpya na anafikiri kwamba “zawadi aliyonayo Bw. Koirala kwa kuwawezesha wengine kwa unyenyekevu na ukweli haitaondoka wa haraka”.

Waandishi wa Habari za Kiraia, Jiandikishe Kupata Video Bure

  23 Februari 2014

Jukwaa linalokusanya video kadri zinavyowekwa mtandaoni linaloitwa Ustream linalota fursa ya kujiandikisha kufungua anuania mpya na pia kuzitangaza kwa ajili ya kuzitumia video hizo kwa ajili ya habari zinazotokea, uanaharakati na hata kwa matumizi ya mengine ya faida kwa jamii. Hivi karibuni Ustream imesaidia chaneli tatu za moja kwa moja...

Kuhusu habari zetu za Muhtasari wa Habari

Hizi ni habari mpya zilizoandikwa kwa muhtasari.