Habari kutoka Muhtasari wa Habari kutoka Mei, 2014
Je, Madaraka ni Matamu Kiasi cha Watawala wa Afrika Kushindwa Kuyaachia?
Gershom Ndhlovu anaangalia sababu za kwa nini watawala wa Afrika hawataki kuachia madaraka: Kumekuwepo na tetesi, dondoo na hata uvumi kuhusu afya au basi udhaifu wa afya ya Rais wa Zambia Michael Chilufya Sata, aliye madarakani tangu Septemba 2011. Tetesi hizi zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii kiasi kwamba serikali...
Changamoto za Elimu kwa Karne ya 21
Mikel Agirregabiria kwa kujifunza kutoka kwenye filamu Dead Poets Society aliweza kubainisha [es] mahitaji ya sasa ya elimu: Elimu katika karne ya 21 yahitaji kushughulikia masuala ambayo hayakuwa bayana siku za nyuma, kama vile wapi unapotaka kuishi au kufanya kazi, kwa kutumia lugha gani au kwa utamaduni upi unaweza kujisikia...
Macau: Watu 3,000 Wazunguka Baraza la Wawakilishi Kukwamisha “Muswada wa Walafi”
Taarifa zaidi zinapatikana kwenyetaarifa yetu ya awali ya GV.
Naibu Waziri Ajinyonga baada ya Kushindwa Uchaguzi Nchini Malawi
Blogu ya City Press inaandika kwamba kujinyonga kwa Godfrey Kamanya, Naibu Wairi wa Malawi, baada ya kushindwa kukitetea kiti chake cha ubunge kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Mei 20, 2014 : Matangazo rasmi ya uchaguzi huo uliofanyika Jumanne bado yanaendelea kutangazwa. Lakini matokeo ya awali ya uchaguzi huo yaliyotangazwa na kituo cha redio yalionyesha...
Uchaguzi wa Malawi 2014
Malawi inapiga kura kumchagua rais siku ya Jumanne Mei 20, 2014. Fuatilia taarifa za moja kwa moja kwenye mtandao wa Twita @Malawi2014 na @MEIC_2014.
Mapigano ya Wanakijiji Kugombea Ardhi Yasababisha Maafa Nchini Madagaska
Blogu ya L'Express Mada ilitoa taarifa kwamba kijiji kizima cha Andranondambo kilichoko Kusini mwa Madagascar kiliharibiwa [fr] kufuatia mapigano ya wanakijiji yaliyosababishwa na mzozo wa kumiliki ardhi. Vita vya wenyewe kwa wenyewe, ambayo ilidumu kwa siku tatu kati ya Mei 20-22, ilipoteza maisha ya wanakijiji wote. Akikumbuka tukio hilo, mmoja...
“Hatujaweka Mkazo vya Kutosha Kwenye Afya ya Vijana”
Ripoti ya hivi karibuni kutoka kwa Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu afya ya vijana duniani inabainisha kwamba: Sababu kubwa za vifo vya vijana duniani ni ajali za barabarani, VVU?UKIMWI, na kujiua. Duniani kote, wastani wa vijana milioni 1.3 walipoteza maisha yao mwaka 2012. Ripoti inaongeza vile vile kuwa :...
Jamaika: Alama Zinapoashiria Kikomo
Blogu ya Active Voice imetoa mkusanyiko wa twiti zenye mitazamo ya kupendekeza ufumbuzi kuhusu kampeni ya #bringbackourgirls inayodai kurudishwa kwa wasichana waliotekwa na magaidi wa Boko Haram.
Simulizi za Jinsia na Wajibu
Kwenye blogu ya EnGenerada kuna tafakari ya kina [es] juu ya ujenzi wa utambulisho wa jinsia na masimulizi yanazyohusishwa na wanawake na wanaume. Wanahitimisha kwamba, licha ya kuwa ndugu katika hali halisi, wanafanya kazi kama utaratibu wa kawaida wa kijamii. Makala iliyopitiwa upya hapa ni sehemu ya pili ya #LunesDeBlogsGV...
Wajibu wa Kisayansi katika Mawasiliano
Katika mfululizo mpya wa Cosmos, Víctor R. Ruíz anaonyesha jinsi ambavyo kutafuta maarifa ya kisayansi limekuwa ni jukumu la kijamii na kisayansi katika nyanja za umma: Kabla na wakati huo, makampuni binafsi na serikali yalikuwa na ajenda ambazo daima hazikuwa zikiambatana na maslaha mapana ya jamii. Makampuni ya mafuta yaliendelea...