· Juni, 2013

Habari kutoka Muhtasari wa Habari kutoka Juni, 2013

Rais Obama Kuitembelea Tanzania

  30 Juni 2013

Rais wa kwanza wa Marekani mwenye asili ya Afrika, Barack Obama anatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam kesho alasiri kwa ziara ya kiserikali. Blogu ya Swahili Time imeweka ratiba ya ziara hiyo ya siku mbili. Issa Michuzi aliweka video inayomwonesha Rais Kikwete wa Tanzania akizungumzia ziara hiyo.

Kufilisika kwa Watu nchini Malaysia

  30 Juni 2013

iMoney.my wametengeneza mchoro unaoelezea takwimu za kufilisika nchini Malaysia. Wastani wa matukio 20,000 ya kufilisika yamerekodiwa mwaka 2012 hiyo na maana kwamba wa-Malaysia 53 wanafilisika kila siku.

Athari za Mazingira kwa Uchimbaji Madini Nchini Indonesia

  13 Juni 2013

Makala iliyochapishwa katika mtandao wa mongabay.com imefichua athari za uharibifu wa kimazingira ziazotokana na shughuli za uchimbaji madini katika maeneo ya vijiji nchini Indonesia. Baadhi ya wanazuoni wanahofia kwamba maeneo mengi nchini Indonesia yana kiwango cha juu kabisa cha zebaki duniani.

Jamaica: Watoto kama Wasanii

  11 Juni 2013

Blogu ya Maonyesho ya Sanaa ya Taifa Nchini Jamaika inayo msisimko kuhusu maonyesho yajayo ya sanaa ya watoto, ambayo yataonyesha “mwitikio wa pekee wa watoto kwa maswali kuhusu udadisi wao na msukumo wa aina tofauti wa ubunifu unaokua.”

China Yadaiwa Kuchimba Dhahabu Kinyume cha Sheria Nchini Ghana

Shirika la Habari la Xinhua limeripoti kwamba raia 124 wa Kichina waliodaiwa kushiriki katika uchimbaji wa madini haramu ya dhahabu walikamatwa na kuwekwa kizuizini nchini Ghana. Serikali ya China imetakiwa kulinda na kuwatetea raia wake. Kwa upande mwingine, maoni yaliyotokana na tukio hilo yaliukosoa unyanyasaji unaofanywa dhidi ya watu wa Afrika katika biashara ya...

Kuhusu habari zetu za Muhtasari wa Habari

Hizi ni habari mpya zilizoandikwa kwa muhtasari.