· Novemba, 2009

Habari kutoka Muhtasari wa Habari kutoka Novemba, 2009

Karibea: Tuzo za Fasihi ya Kifaransa

Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, katika makala hii kutoka Haiti, na hii kutoka Guadeloupe na hii...

India: Usawa

  15 Novemba 2009

“Takriban asilimia 15 ya watu ambao ni viongozi wa siasa na watumishi wa serikali, kwa kupitia vitendo vya kifisadi, wamejilimbikizia asilimia 85 ya utajiri wote wa India, na kuwaachia asilimia 15 tu ya utajiri huo asilimia 85 ya wananchi,” anasema Ram Bansal katika blogu ya India in Peril.

Jordan: Barua kwa MBC

M-jordan Ola Eliwat, kutoka Cinnamon Zone, anaandika barua ya wazi kwa makapuni ya televisheni ya MBC. Katika barua hiyo anaandika: “Na tafadhali fikirieni kufunga 90% ya idhaa zenu, nadhani itakuwa hisani KUBWA kwa taifa la Kiarabu!”

Kuhusu habari zetu za Muhtasari wa Habari

Hizi ni habari mpya zilizoandikwa kwa muhtasari.