Habari kutoka Muhtasari wa Habari kutoka Januari, 2014
UBUNIFU: Makontena Yatumika Kama Hosteli za Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Ulaya
Ili kuondoa uhaba wa hosteli kwa ajili ya wanafunzi unaovikabili vyuo vikuu barani Ulaya, baadhi ya vyuo vikuu nchini Denmaki, Ujerumani, Ufaransa (Le Havre) [fr] na Uhispania vimejaribu kubadili makontena na kuyafanya yawe hosteli za wanafunzi. Makontena yanaonekana kufaa kwa sababu hayana gharama kubwa na yanazoeleka kirahisi. Hata hivyo, taasisi kadhaa tayari zimeibua...
Shindano la Kuchochea Uanzishwaji wa Biashara Mpaya Nchini Madagaska
Harinjaka, mwanzilishi wa mradi wa Habaka na mwanablogu anayeishi Madagaska, ameanzisha Shindano la biashara mpya Antananarivo 2014 [fr] lenye lengo la kuchagua na kuunga mkono wazo la biashara nchini Madagaska. Anaamini kwmaba kuna mustakabali mzuri kwa ujasiriamali na ubunifu [fr] nchini Madagaskari. Hapa unaweza kuona tangazo la tukio hilo[fr] :
Mwaliko wa Mapendekezo ya Tuzo za Blogu Nchini Kenya 2014
Waandaaji wa Tuzo za Blogu nchini Kenya 2014, ambao ni Umoja wa Wanablogu nchini humo (BAKE) kwa sasa wanakaribisha mapendekezo ya wawaniaji wa tuzo hizo mpaka Februari 10, 2014. Watumiaji wanaweza kupiga kura kwa njia ya mtandao kuanzia Machi 1, mpaka April 30, 2014 kupendekeza blogu wanazoona kuwa ni bora...
Trinidad & Tobago: Mambo Madogo Yaweza Kuleta Utofauti
ban-d-wagonist aweka video yenye “maoni rahisi ya namna ambavyo raia wa kawaida wanavyoweza kuijenga Trinidad na Tobago yenye mafanikio.”
PICHA: Kimbunga BEJISA Chasababisha Uharibifu Mkubwa katika Visiwa vya Reunion
Januari 2, Kimbunga Bejisa kilisababisha uharibifu mkubwa katika kisiwa cha Reunion kilicho chini ya mamlaka ya Ufaransa. Mtu mmoja alifariki na wengine 15 kujeruhiwa vibaya, huku idadi ya nyumba zinazokadiriwa kufikia 82,000 zikiripotiwa kukosa huduma ya nishati ya umeme. Kimbunga hiki kimeshatulia na hali ya hatari imeshatangazwa kisiwani humo. Zifutazo...
Rais wa Korea Kusini Aapa Kupambana Uzushi Unaoenezwa katika Mitandao ya Kijamii
Je, serikali ya Korea Kusini imejiandaa kwa kufuatilia mitandao ya kijamii? Matamshi ya hivi karibuni ya Rais Park (full transcript [ko]) yamewashitua wa-Korea wanaotumia mtandao. Park, akiwalenga “uvumi ule unaosambaa kupitia mitandao ya kijamii”, alisema “kama serikali ikiachia mambo haya yakaendelea, itakuwa ghasia nchi nzima” na kuongeza “kumbukeni mamlaka za nchi zinahitaji...
Uvumbuzi: Kompyuta Inayotumia Nishati ya Jua Nchini Mali
Kama sehemu ya mfululizo wetu juu ya teknolojia na ugunduzi unaofanyika Afrika, hivi karibuni tulionyesha Mashine ya Kuchapishia picha zenye umbo halisi yaani 3D iliyotengenezwa kutokana na taka pepe nchini Togo na mashine ya kukagua usahihi wa maneno katika lugha ya spell ki-Bambara . Leo, tunawaletea kompyuta ya kwanza kutumia...
Wa-China Wametafuta Nini Zaidi Mtandaoni mwaka 2013
Mtandao wa kutafutia habari mtandaoni nchini China uitwao Baidu umetoa orodha ya maneno yaliyotumika zaidi kusaka habari. Orodha ya maneno kumi yaliyotumika zaidi ni kama ifuatavyo: Hali ya Hewa Taobao (tovuti ya kufanyia manunuzi ya mtandaoni nchini China) Wu Dong Qian Kun (kitabu cha mtandaoni cha Li Hu) The Tang Door...
Uajemi: Washairi Wawili Watiwa Nguvuni
Washairi Mehdi Mousavi na Fatemeh Ekhtesari wametokomea nchini Uajemi. Kwa mujibu wa taarifa za habari, washairi hao wamewekwa kizuizini tangu mwanzoni wa mwezi Desemba. Zaidi ya watu mia mbili wametia saini hati ya malalamiko mtandaoni na kutoa wito kwa Umoja wa Mataifa kuchukua hatua kuhusiana na hali za wanaharakati wa...