Habari kuhusu Tanzania

Kupigia Kura Maajabu Saba ya Dunia barani Afrika

  27 Disemba 2012

Shindano la kila mwaka limezinduliwa kwa ajili ya watu kupiga kura kuchagua maajabu saba yaliyo bora zaidi barani Afrika. Na tayari upigaji kura umeshaanza. Baadhi ya maajabu ya asili yaliondolewa katika orodha ya mwisho ya kupigiwa kura na hivyo baadhi ya wanablogu waliongeza mapendekezo yao katika blogu zao. Tazama baadhi ya picha hapa:

Mradi wa Tafsiri: Kauli ya Linda Uhuru wa Intaneti Ulimwenguni

GV Utetezi  20 Novemba 2012

Katika siku saba zijazo, Wafasiri wa Kujitolea wa Mradi wa Lingua wa taasisi ya Global Voices watakuwa wakitafsiri makala maalumu ambayo ni harakati ya utetezi unaofanywa na umma mtandaoni na ambao unasaidia kulinda haki za watu kwenye mitandao ya intaneti na kuzitaka serikali zilizo wanachama wa Muungano wa Kimataifa wa...

Tanzania: Mgomo wa Walimu Watikisa Nchi

  31 Julai 2012

Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kufanyika zoezi la sensa, walimu nchini Tanzania wako katika mgomo kuishinikiza serikali kuwalipa madai yao pamoja na kuboresha mishahara yao. Hatua hiyo imevuta hisia za watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii wanaojadili madhara ya mgomo huo.

Afrika: Usanii wa Kisasa wa ki-Afrika Mtandaoni

  31 Julai 2012

Usanii Afrika blogu inayoonyesha usanii wa kisasa wa ki-Afrika: Usanii Afrika ni blogu iliyozaliwa kutokana na upenzi. Akiwa amezaliwa na kipaji cha ubunifu yeye mwenyewe, mwanablogu, Kirsty Macdonald amekuwa na mahusiano ya karibu na masuala ya sanaa na kujieleza”

Tanzania: Kufungiwa ‘Mwanahalisi’, uhuru wa habari mashakani?

  30 Julai 2012

Mnamo tarehe 30 Julai, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Msajiri wa Habari ilitangaza kulifungia kwa muda usiojulikana gazeti la Kiswahili linalotoka mara moja kila wiki la 'MwanaHalisi'. Ulimwengu wa habari umepokea taarifa hiyo kwa mshtuko mkubwa. Hivi ndivyo wanaharakati wa mtandaoni wanavyoeleza hisia zao kuhusu tangazo hilo.

Tanzania: Mwigizaji Nyota wa Filamu, Steven Kanumba, Afariki Dunia

  13 Aprili 2012

Tanzania ilimuaga mmoja wa wasanii wake maarufu na nyota wa tasnia ya filamu, Steven Kanumba, kwa maziko yaliyogubikwa na majonzi mazito mnamo tarehe 11 Aprili 2012. Alifariki alfajiri ya Jumamosi, akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kile kilichodaiwa kuwa ugomvi wa kimapenzi na rafiki yake wa kike aitwaye Elizabeth Michael kwa jina maarufu “Lulu”.

Tanzania: Majumuisho ya Habari za Uchaguzi Mkuu wa 2010

  30 Oktoba 2010

Mnamo tarehe 31 Oktoba 2010, Watanzania watashiriki katika uchaguzi wa Rais wa Muungano, Rais wa Zanzibar pamoja na Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Huu ni mjumuisho wa yale yaliyojiri katika blogu mbalimbali kuhusiana na uchaguzi huo.