Habari kuhusu Tanzania
GV Face: Magaidi Wanatwiti? Shambulio la Westgate
Toleo la juma hili la mfululizo wa Mazungumzo yetu ya GV Face kupitia Google Hangout, tunajadili wajibu wa uandishi wa kiraia baada ya tukio la kigaidi la Kenya.
Bunge la Tanzania Lageuka Uwanja wa Masumbwi
Siku za hivi karibuni, Mbunge wa Bunge la Tanzania alijikuta katika wakati mgumu pale alipokabiliana kwa nguvu na majibizano na maafisa wa usalama wa Bunge. Si mara ya kwanza kwa hali ya mambo kuishia kwa machafuko katika Bunge la Tanzania.
Tanzania: Uchaguzi Mdogo wa Madiwani Arusha Waipa CHADEMA Ushindi
Uchaguzi mdogo wa Madiwani Jijini Arusha umefanyika kwa amani leo Jumapili Julai 14. Mtandao maarufu wa Jamii Forums uliripoti yanayoendelea Arusha wakati wote na baada ya uchaguzi. Blogu ya Wavuti imeweka matokeo ya uchaguzi huo pamoja na picha mbalimbali za uchaguzi: Huku Tume ya Uchaguzi ikisubiriwa kuwatangaza rasmi washindi, taarifa...
Je, Ziara ya Obama Barani Afrika ni Neema au Hasara?
Rais wa Marekani Barack Obama amemaliza ziara yake ya siku sita katika nchi tatu za Kiafrika, Senegali, Afrika Kusini na Tanzania, mnamo Julai 2, 2013. Obama alitangaza mradi mpya, "Umeme Afrika", kukuza matumizi ya umeme mara dufu katika nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara. Maoni ya watu duniani kote juu ya umuhimu na matokeo ya ziara hiyo yamegawanyika mno.
Obama Barani Afrika: Vita ya Kibiashara na China?
Rais Obama ametembelea bara la Afrika kwa ziara iliyokuwa imepangwa kati ya tarehe 26 mpaka Julai 3, 2013. Hivi karibuni alikuwa nchini Afrika Kusini baada ya kutembelea Senegali na baadae aliitembelea Tanzania. Wachambuzi wengi wanaoiona safari hiyo kama mpango wa kushindana , kama jaribio la Marekani kupambana na mafanikio ya kiuchumi ya China katika nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Watanzania Waitafakari Ziara ya Obama Iliyosubiriwa kwa Matumaini Makubwa
Dar es Salaam, ambao ni mji mkuu wa kibiashara wa Tanzania, unarejea katika hali yake ya kawaida baada ya siku mbili za kuwa mwenyeji wa mtu anayeaminika kuwa mwenye mvuto mkubwa duniani, Rais wa Marekani, Barack Obama. Mitaa ya jiji la Dar Es Salaam ilihanikizwa na picha za Rais huyu.
Rais Obama Kuitembelea Tanzania
Rais wa kwanza wa Marekani mwenye asili ya Afrika, Barack Obama anatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam kesho alasiri kwa ziara ya kiserikali. Blogu ya Swahili Time imeweka ratiba ya ziara hiyo ya siku mbili. Issa Michuzi aliweka video inayomwonesha Rais Kikwete wa Tanzania akizungumzia ziara hiyo.
Mfululizo wa Tamthilia ya Runinga ya Nchini Tanzania
The Team Tanzania (Timu Tanzania) ni mfululizo wa Tamthilia ya Runinga yenye kuzungumzia: […] Bi. Wito, mwalimu mahiri wa somo la uraia, anaigeuza kabisa mitazamo ya vijana makinda watatu anapowauliza maswali mazito mfano “Wewe ni nani”? vijana wale wenye umri wa miaka 16, waliofahamiana vyema tangu wakikua. Katika kuingia katika...
Michoro ya Dar: Sanaa kwa Maendeleo Endelevu
Dar Sketches (Michoro ya Dar) ni sehemu ya mradi unaoanzia ngazi ya Mtaa jijini Dar Es Salaam, Tanzania ulioanzishwa na msanii na mchoraji Sarah Markes: Ni katika kuenzi urithi wa kitamaduni na wa sanaa ya ubunifu wa majengo kwa jiji la Dar Es Salaam sambamba na juhudi za kukuza uelewa...
Tanzania: Ghorofa Laporomoka jijini Dar Es Salaam
Pernille anaweka picha mtandaoni zinazoonyesha ghorofa lililoporomoka jijini Dar Es Salaam, Tanzania siku ya Ijumaa, 29 Machi 20013: “Karibu kabisa na jengo hilo kuna uwanja wa kandanda unaotumiwa na watoto. Zaidi ya watu 60, pamoja na watoto, wanaripotiwa kupotea kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha ITV. Hakuna kauli rasmi...