Habari kutoka Muhtasari wa Habari kutoka Septemba, 2014
Uimarishaji wa Amani ya Kudumu Jamhuri ya Afrika ya Kati
Wakati Umoja wa Mataifa ukizindua mpango wake wa kulinda amani kwa kutuma wanajeshi 1,500 nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, wafuatiliaji wachache wanajiuliza ni kwa nini uamuzi huu ulichukua muda mrefu pamoja na kuwepo kwa wahanga wengi wa machafuko. Les Cercles nationaux de Réflexion sur la Jeunesse (CNRJ) ni shirika lisilo...
Wanabogu wa Togo Wamtania Rais Kufuatia Ujumbe wa Bango Barabarani
Mtu mmoja alitaka watu wajue kwamba alikuwa na shukrani kwa ukarimu wa Rais wa Togo Faure Gnassingbé. Wiki hii, bango kubwa liliwekwa jijini Lomé, Togo kusifia kitendo cha Rais kutoa chakula cha mchana kwa watoto. Bango hili linaloonekana hapa chini lina maneno haya kwa lugha ya Kifaransa:” Asante sana Baba Faure...
Jinsi Wanablogu Walifikia Gerezani kwa Kuandika Kuhusu Haki za Binadamu Nchini Ethiopia
Melody Sundberg anachambua uhuru wa kujieleza nchini Ethiopia baada ya wanablogu wa Ethiopia waliokamatwa kukaa siku 100 gerezani: Ethiopia ina idadi ya watu 94,000,000 na ni nchi ya pili yenye wakazi wengi katika bara la Afrika. Hata hivyo, hailingani na mahojiano ya Endalkhachew Chala kupitia Global Voices, kuwa na gazeti...
Majadiliano na Picha za Mkutano wa Highway Africa 2014
Mkutano wa Highway Africa 2014 ulifanyika kuanzia tarehe 7-8 Septemba, 2014 kwenye Chuo Kikuu cha Rhodes, Grahamstown, Afrika Kusini. Maudhui ya mkutano huo yalikuwa Mitandao ya Kijamii -kutoka pembezoni kwenda kwenda kwenye vyombo vikuu vy habari. Angalia picha na mzungumzo kuhusiana na mkutano huo hapa.
Habari Mpya za Mgogoro wa Kisiasa Lesotho Kupitia Twita
Mfuatilie @nthakoana (Nthakoana Ngatane) kupata habari mpya zinazohusu mgogoro wa kisiasa nchini Lesotho. Nthakoana Ngatane ni mwandishi, msemaji, mwimbajii, mwigizaji na mwakilishi wa SHirika la Habari la Utangazaji la Afrika Kusini nchini Lesotho. Mnamo tarehe 30 Agosti 2014, Waziri Mkuu wa Lesotho Tom Thabane alidai kulikuwa na jaribio la kumpindua...
Je Kulikuwa na Jaribio la Mapinduzi Nchini Lesotho?
Sikiliza sauti inayoelezea kile hasa kinachoendelea nchini Lesotho kufuatia madai ya mapinduzi ya kijeshi: Waziri mkuu amekimbilia nchini Afrika Kusini na anasema ni mapinduzi ya kijeshi. Jeshi la Lesotho linasema sio mapinduzi. Siasa zinazua utata. African Defence Review inazungumza na KRISTEN VAN SCHIE wa SADC na mwandishi DARREN OLIVIER kuuliza...
Nzige Wavamia Mji Mkuu wa Madagaska
#valala pic.twitter.com/YHzOx5Q8QU — Vaintche Rahouli (@vincraholi) Agosti 28, 2014 Watumiaji-mtandao wa Twita na Facebook kutoka mji mkuu wa Madagaska, Antananarivo, wamepachika picha kadhaa za nzige wakivamia mji. Uvamizi wa nzige sio tukio la ajabu nchini Madagaska, hasa baada ya dhoruba za kitropiki, lakini sio kawaida katika miji mikubwa. Nzige wanaweza...
Watu 12 Hufa na Waniger 27,000 Huachwa Bila Makazi Kutokana na Mafuriko
Mvua kubwa na mafuriko nchini Niger yamewaua watu 12 na kuacha maelfu bila makazi. Mito katika Niamey na maeneo ya karibu imefurika na kuharibu maelfu ya nyumba. Katika kanda, uharibifu wa ardhi na kilimo pembezoni mwa ardhi huzidisha hatari ya kwamba matukio yaliyokithiri yanaweza kubadilika kuwa maafa ya asili. Baadhi ya...