Habari kuhusu Utawala kutoka Machi, 2010
Siku ya Ada Lovelace: Kuwapongeza Wanawake Wanajishughulisha Kupigania Teknolojia na Uwazi Ulimwenguni
Katika kusherehekea Siku ya Ada Lovelace tunawaletea makala fupifupi kuhusu wanawake kadhaa walio sehemu mbalimbali duniani ambao hutumia teknolojia ili kuzifanya serikali ziwe wazi na zinazowajibika zaidi.
Global Pulse 2010: Mwaliko wa kuzungumza na watoa uamuzi mtandaoni
Kuanzia tarehe 29 hadi 31 Machi, vuguvugu linalojulikana kama Global Pulse 2010, yaani Mapigo ya Moyo ya Ulimwengu 2010, linakusudia kuwakusanya jumla ya watu 20,000 kupitia mtandao ili wafanya mazungumzo kuhusu mada mbalimbali kuanzia zinazohusu maendeleo ya binadamu hadi sayansi na teknolojia.
China: Uchi Ulio Rasmi
Serikali moja ya mji huko katika Jimbo la Sichuan sasa inaitwa “Serikali ya Kwanza nchini China Iliyo Uchi kabisa” baada ya kuwa maafisa wa mji huo kuweka mishahara na matumizi...
Martinique: Uchaguzi, utata na kugomea uchaguzi
Jumapili ya tarehe 14 Machi, raia wote wa Ufaransa wakiwemo wale wa idara za ng’ambo za Ufaransa walitakiwa kupiga kura... Lakini michakato miwili ya uchaguzi katika kipindi cha miezi mitatu inaweza kuwachosha 55.55% ya wapiga kura wa Martinique ambo waliamua kubaki majumbani.
Thailand: Utulivu Kabla ya Kimbunga?
Maandanmano ya kuipinga serikali ya Machi 12 yalimalika salama huku kundi la Mashati Mekundu likiapa kurejea tena mitaani mwishoni maw juma hili ili kuendelea kushinikiza kuvunjwa kwa bunge na kuitisha uchaguzi mkuu. Wanablogu na watumiaji wa Twita wanatoa maoni yao.
Sudani: Je, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Itafanya Kazi?
Jarida la The Financial Times liliripoti hivi karibuni kuwa mpango wa mamilioni ya dola wa Benki ya Dunia wa kusambaza kompyuta na upatikanaji wa Intaneti huko Juba, mji mkuu wa Sudani ya Kusini, umeshindwa. habari hizi zinazua swali: kelele zinazoambatana na teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) zina uhalali?
Naijeria: Ghasia Zalipuka Huko Jos Kwa Mara Nyingine
Huko Jos, machafuko yanaelekea kujitokeza katika mizunguko inayozidi kuwa midogo: machafuko mabaya yaliukumba mji huo mwaka 1994, 2001, 2008, na – hata miezi miwili iliyopita – mnamo mwezi Januari 2010. Mgogoro wa sasa unasemekana kuwa ulianza katika tukio la kisasi kilichotokana na uharibifu uliotokea mwezi Januari, na, kama ilivyokuwa kwenye machafuko yaliyopita, mapambano ya sasa huko Jos yamekuwa yakipiginwa katika misingi ya kidini.
Iraki: Ni Siku ya Uchaguzi Kwenye Twita
Ni siku ya uchaguzi nchini Iraki na ulimwengu wa Twita umekuwa uking’ong’a na habari mpya mpya tangu mapema asubuhi. Waandishi wa habari na wanahabari wa kijamii walijaribu kutumia Twita ili kutupasha habari kuhusu mambo yanavyotukia nchini humo.