· Septemba, 2008

Habari kuhusu Utawala kutoka Septemba, 2008

Sheria inapokwaza haki za binadamu …

  29 Septemba 2008

Mtoto mwenye umri wa shule ya msingi aliyepatikana nje ya ndoa huko Zhuhai, kusini mwa China, hakubaliwi kujiunga na shule, kwa sababu mama yake hawezi kulipa faini kubwa ya kuwa na "mwana haramu", habari hii inasimuliwa na bloga, Han Tao.

Msumbiji: Mgogoro wa Kisiasa Katika Jimbo la Kati la Beira

Waunga mkono wa Renamo wenye hasira walimwagika katika mitaa ya Beira ili kupinga uamuzi wa chama wa kumbadilisha Meya aliyeko madarakani Bwana Davis Simango na kumuweka Manuel Pereira kama mgombea wa kiti cha serikali ya manispaa katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Mwezi Novemba 2009. Mwanahistoria Egidio Vaz anaandika barua ya wazi kwa Rais wa Renamo, Bwana Alphonso Dhlakama katika blogu yake.

Jordan: Ubloga wa Video wa Malkia Rania

  12 Septemba 2008

Chombo cha habari cha Blogger Times kinachoendeshwa na mabloga wa Kiarabu, kimemtaja Malkia Rania wa Jordan kuwa bloga maarufu zaidi wa video za kutoka Uarabuni katika chombo cha Video mtandaoni, YouTube, kufuatia mafanikio ya mlolongo wa video za YouTube aliouanzisha kuondoa dhana potofu dhidi ya Waarabu.

Venezuela: Wahindi wa Yukpa, Chavez na Mgogoro wa Ardhi

  6 Septemba 2008

Picha za video zinazotumwa kwenye mtandao wa internet na vyombo vya habari vya kiraia zinaonyesha yale yanayojiri kuhusu mgogoro unaoibuka nchini Venezuela kati ya Wahindi wa jamii ya Yukpa wanaoishi katika milima ya Perijá, wamiliki wa ardhi na Rais Chávez. Mgogoro huu kuhusu mipaka ya ardhi umekuwapo kwa takribani miaka 30, yaani tangu pale vikosi vya jeshi vilipowandoa kwa nguvu wanajamii wenyeji ya Ki-Yukpa na kuwapa ardhi hiyo wamiliki wapya walioanzisha mashamba makubwa ya mifugo, hasa ng'ombe, ambao wameendelea kuitumia ardhi hiyo tangu wakati huo.