Habari kuhusu Utawala kutoka Agosti, 2013
Iran: Mwanablogu Aliyefungwa Jela Afanya Mgomo wa Kutokula
Hossein Ronaghi Malki mwanablogu anayetumikia kifungo cha miaka 15 jela alianza mgomo wake wa kutokula kuanzia wiki iliyopita. Kwenye mtandao wa Facebook kampeni imeanzishwa yenye lengo la kummwuunga mkono.
China: Kisasi au Haki?
Kashfa ya ngono ya hivi majuzi inayowahusisha majaji wawili maarufu wa Shanghai iliwekwa hadharani na mfanyabiashara Ni Peiguo anayeamini kuwa mmoja wa majaji hakutoa hukumu ya haki katika kesi ya kampuni anayohusika nayo. Alichukua uamuzi wa kulipiza kisasi kufuatia hasara ya fedha kwa kumfuatilia hakimu kwa mwaka na hatimaye kufichua kashfa yake ya ngono. Mtandao...
Iran: Waziri Mpya wa Kigeni Yupo Kwenye Mtandao wa Facebook
Waziri mpya wa Uhusiano wa Kimataifa wa Iran Mohammad Javad Zarif ana ukurasa wa Facebook ambapo huutumia kujibu maswali. Anasema “Mimi na watoto wangu huuhuisha (kuweka habari mpya) ukurasa huu.” Ukurasa huo una zaidi ya wafuatialiaji 79,854 walioupenda (wakati wa kutafsiriwa kwa posti hii). Mtandao wa Facebook hudhibitiwa nchini Iran lakini ndio...