· Juni, 2012

Habari kuhusu Utawala kutoka Juni, 2012

Misri: Yatambulisha Kipimio cha Morsi

Baada ya miaka 32 ya Hosni Mubarak, Misri imepata rais mpya Mohamed Morsi, na pia kitumizi cha kufuatilia utendaji pamoja na maendeleo ya kutimiza ahadi kuu 64 alizozitoa rais huyo mteule wakati wa kampeni za uchaguzi nchini humo.

26 Juni 2012

Kenya: Wanaharakati wapigana vita dhidi ya ufisadi kwa intaneti

I Paid a Bribe ni njia mojawapo inayotumiwa na wanaharakati dhidi ya ufisadi nchini, kwa kutumia teknolojia mpya ili kuwawezesha kupata ripoti za utoaji wa hongo.' I paid a Bribe' imefuatia muundo wa ‘India Anti-Corruption Portal (IPAB)' na ni ushirkiano kati ya IPAB na Wamani Trust ya Kenya ili kuleta IPAB katika Afrika Mashariki na Kati.

7 Juni 2012

Uganda: Je, Uganda inageuka kuwa dola ya kifalme?

Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni amekuwa madarakani tangu mwaka 1986. Majuma machache yaliyopita, wananchi walianza kudodosa habari za nani hasa atamrithi kama ataamua kutokugombea kwa awamu ya nne mwaka 2016. Tetesi zinadai kwamba rais anamwunga mkono mkewe, Waziri wa mambo ya Karamoja kurithi kiti cha rais.

3 Juni 2012