Habari kuhusu Utawala kutoka Aprili, 2014
Ni “Udhaifu” wa Serikali, Yasema Ripoti ya Ajali ya Kivuko cha Korea Kusini
Zimetimu siku 14 tangu kivuko cha Sewol kizame na watu 205 wamethibitika kupoteza maisha. Wanasiasa wanatumia tukio hilo na habari zisizosahihi za vyombo vya habari kuchochea hasira miongoni mwa Wakorea Kusini.
Changamoto ya Kuhuisha Orodha ya Wapiga Kura
Uchaguzi mkubwa zaidi duniani uko mbioni nchini India na mwanablogu Anuradha Shankar kwenye blogu yake ya “A Wandering Mind” anabainisha changangamoto halisi za kuboresha daftari la wapiga kura tayari kwa matumizi.
Magonjwa ya Afya ya Akili Hayapewi Kipaumbele Nchini Cambodia
Akiandika kwa niaba ya Southeast Asia Globe, Denise Hruby aliripoti jinsi wagonjwa wa akili katika maeneo mengi ya vijijini vya Cambodia wanavyofanyiwa: …Wagonjwa wa akili bado hutibiwa na waganga wa jadi, ambao lengo lao ni kuwatoa pepo wabaya kwa kuchoma ngozi, au kwa wafanyakazi wasio na ujuzi wa chumba kimoja...
VIDEO: Wanafunzi wa Iran Wavuruga Hotuba ya Mgombea Urais wa Chama Tawala
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Amirkabir kilichopo mjini Tehran, nchini Iran waliimba nyimbo zenye vibwagizo vinavyomwuunga mkono Mir Hussein Mousavi na Mehdi Karroubi, ambao ni viongozi wa vyama vya Upinzani nchini humo waliowahi kuongoza maandamano ya Green Movement.
Serikali Mpya ya Waziri Mkuu Roger Kolo Yatangazwa Nchini Madagaska
Mtandao wa Tananews nchini Madagascar umechapisha orodha kamili ya mawaziri 31 wa serikali mpya ya Madagaska [fr]. Mitsangana Madagascar anasema kwamba orodha hiyo ina wanawake 6 na kuwa mawaziri 7 walikuwa kwenye baraza[fr] la serikali iliyopita ya mpito. Waziri mkuu wa zamani Beriziky aliitakia serikali kila la heri kwenye mtandao...
Chanzo cha Maji nchini China Chawekwa Kemikali Inayosababisha Kansa
Benzene, kemikali inayosababisha kansa kwa haraka kabisa, imegundulika kuwepo kwenye chanzo cha maji cha Jiji la Lanzhou , wakati fulani ilipimwa na kukutwa kwa kiwango cha mara 20 zaidi ya kile kinachofahamika kuwa ni salama kwa matumizi.
Blogu ya Tunisia Yazindua Jukwaa la ‘Kuvujisha Taarifa Nyeti’
Blogu ya Tunisia iliyowahi kushinda tuzo iitwayo Nawaat imezindua jukwaa lake la kuvujishia taarifa nyeti: Nawaat Leaks.
Asilimia 20-40% ya Fedha Katika Sekta ya Maji Barani Afrika Hupotelea kwa Utoaji Rushwa
Mustapha Sesay, Balozi wa Uadilifu wa Afrika Magharibi aliandika kuhusu ufisadi katika sekta ya maji kwenye mtandao wa Waandishi wa Habari wa WASH wa Afrika Magharibi : Suala la upatikanaji wa maji safi na kwa bei nafuu ni haki ya kibinadamu lakini hii haijapewa kipaumbele inavyohitajika sana. Utoaji rushwa katika...
Mgogoro Usiopewa Uzito Stahiki Nchini Burundi
Wakati nchi jirani ya Rwanda inagonga vichwa vya habari na maadhimisho ya mauaji ya kimbari ya mwaka wa 1994 na kuongezeka kwa mvutano na Ufaransa, Burundi imeharibiwa katika kupuuzwa kwa mgogoro wa kisiasa na dalili za vurugu zinazoweza kusababisha mapigano mapya ya Wahutu na Watutsi. Tshitenge Lubabu nchini Burundi anatoa...
Kwa Nini Rais wa Madagaska Hajatangaza Uteuzi wa Waziri Mkuu
Rais mpya wa Madagaska Hery Rajaonarimampianina alichaguliwa kuwa raia mnamo Desemba 20, 2013. Miezi michache baadae, bado hajatangaza uteuzi wa waziri mkuu wa serikali yake mpya. Wachunguzi wengi wanashangaa kwa nini imechukua muda mrefu. Mwanablogu wa Kimalagasi Michael Rakotoarison ana maoni tofauti kuhusiana na hali hiyo; hoja yake ni kuwa huenda...