· Julai, 2010

Habari kuhusu Utawala kutoka Julai, 2010

Niger: Njaa ya Kimya Kimya

Janga la njaa ambalo kwa kiasi kikubwa haliripotiwi ipasavyo huko Sahel limechukua sura kubwa ya kutisha kufuatia kiasi cha watu milioni 2.5 nchini Naija hivi sasa kuathirika na uhaba wa chakula. Wanablogu nchini Naija wanatafakari janga jingine la chakula baada ya lile la mwaka 2005.

31 Julai 2010

Thailand: Vurugu Zinazotokana na Ujumbe Mfupi wa Maneno wa Waziri Mkuu

Wakati Waziri mkuu wa Thailand Abhisit Vejjajiva alipotwaa madaraka mwaka 2008, alituma ujumbe mfupi wa maneno kwa mamilioni ya wateja wa simu za viganjani wa Thailand akiwataka wawe na umoja. Hivi sasa anakabiliwa na makosa ya ufisadi kwa kupokea "zawadi" kutoka mashirika ya mawasiliano. Kadhalika anashutumiwa kwa kuvunja mipaka ya ya faragha za wateja wa simu za viganjani.

27 Julai 2010

Ivory Coast: Mwanablogu na Mwandishi wa Habari Théophile Kouamouo Akamatwa Pamoja na Timu Yake Tangu Julai 13

Waandishi wa habari watatu wa Le Nouveau Courrier d'Abidjan walitiwa mbaroni na polisi baada ya kukataa kueleza vyanzo vya habari vya uandishi wao wa kipelelezi kuhusu biashara ya usafirishaji kahawa na kakao kwenda nje ya nchi. Yafuatayo ni maoni kutoka kwa raia na vyombo vya habari nchini Ivory Coast huku wenzao watatu wakiendelea kupigania kuachiwa kwa wanahabari hao.

19 Julai 2010

Naijeria: Nani Amemfanya Rais Abadili Msimamo — Facebook au FIFA?

Baada ya kupokea mamia ya maoni kwenye ukurasa wake wa Facebook page, Rais wa Naijeria alibadili uamuzi wake tata wa kuifungia timu ya taifa ya nchi hiyo. Lakini je ni kweli kwamba kubadilika huku kwa moyo wa Jonathan kulitokana na maoni ya raia waliopaaza sauti zao zenye hasira katika Facebook? Au ulitokana na msukumo wa shirikisho lenye nguvu la mpira wa miguu?

13 Julai 2010

Angola: Hapo Zamani za Kale Katika Roque Santeiro

Maendeleo yanayoukumba mji wa Luanda unaliwajibisha moja ya eneo la biashara linalotembelewa zaidi mjini humo, eneo ambalo hutengeneza maelfu ya dola kwa siku. Soko la Roque Santeiro limo mbioni kufunga "milango" yake na kufunguliwa katika eneo la kisasa na lenye hadhi, huko Sambizanga.

3 Julai 2010