Habari kuhusu Utawala kutoka Oktoba, 2009
Malayasia: Serikali ya Jimbo Yaja na Sera ya ‘Msala Mmoja’
Kwa kuiga chapa ya Malaysia1, serikali ya Jimbo la Terengganu hivi majuzi ilikuja na sera ya ‘msala 1’ kama hatua kwa walimu na wanafunzi (wa jinsia moja) kuchangia misala (vyoo) ili kukuza hisia za umoja. Kumekuwepo na maoni mchanganyiko katika ulimwengu wa blogu kuhusiana na sera hii.
Japan: Uchunguzi Mpya Juu ya Umaskini Waharibu Soga za Utajiri
Mjapani mmoja kati ya sita anaishi katika umasikini inasema ripoti mpya ya Wizara ya Ustawi wa Jamii [en]. Kwa mujibu wa takwimu za OECD, Japan ina kiwango kikubwa zaidi cha...
Bhutan: Mpito Usio na Mikwaruzo Kuelekea Demokrasi
Tshering Tobgay, kiongozi wa chama cha upinzani katika Bunge la Taifa la Bhutan, anatoa maoni kuwa: “mpito wetu kuelekea demokrasi, kwa hakika, umetukia bila mikwaruzo. Umetukia bila mikwaruzo kiasi kwamba...
Marekani: Wanandoa wa rangi tofauti wanyimwa cheti cha ndoa
Juma lililopita huko Hammond, Louisiana, wapenzi wawili walituma maombi ya kibali cha kufunga ndoa na walikataliwa kwa misingi ya rangi zao tofauti. Afisa wa kutathmini na kuandikisha nyaraka (Muamuzi wa Amani) alidai kuwa “ndoa baina ya watu wa rangi hazidumu” na alisema kuwa anafanya hivyo “kwa ajili ya watoto.”
Trinidad & Tobago: Mtrini Mpaka Kwenye Mifupa?
“Kila siku ambayo ninapitia habari ninazidi kushawishika kuwa ninataka kuachana na klabu ya ‘Mimi ni Mtrini’ na kwenda sehemu nyingine”: Coffeewallah ameshachoka na kila kitu kuanzia uhalifu mpaka kodi.
Namibia: Kampeni ya Kukomesha Chanjo za Lazima
Kampeni ya kukomesha Chanjo kwa kulazimishwa nchini Namibia imezinduliwa: “ umoja wa Asasi za kijamii umetoa wito kwa Wanamibia wote kujiunga na kampeni ya kulaani chanjo kwa wanawake waishio na...