Habari kuhusu Ethiopia

Utani Mitandaoni: Siku ya Wajinga Nchini Ethiopia

  1 Aprili 2014

Wa-Ethiopia kwenye mtandao wa twita wanasherehekea siku ya wajinga duniani kwa kutangaza habari bandia ambazo zinaiga uongo unaotangazwa na vyombo vya habari vya serikali. Raia mmoja wa Ethiopia anayetwiti: “Wanatangaza uongo wa mchana siku 365 za mwaka, ngoja twarudishie dozi ya kuwatosha yenye habari za uongo kadri tunavyoweza”. Wafuatilie ili...

Ethiopia: Mwanablogu Ahukumiwa Miaka 18 Jela kwa “Kuvunja Katiba”

GV Utetezi  4 Mei 2013

Mnamo Mei 1, Mahakama Kuu ya Ethiopia ilitoa hukumu kali kwa mwandishi aliyeshinda tuzo Eskinder Nega, ambaye sasa atatumikia kifungo cha miaka 18 jela. Mohamed Keita wa Kamati ya Kuwalinda Waandishi anasema, “Kushitakiwa na hatimaye kutiwa hatiani kwa Eskinder na waandishi wengine ni dalili za utawala unaoogopa maoni ya raia wake.”

Kitabu-pepe Kipya cha GV: Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko

  30 Disemba 2012

"Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko",  kinakupa mtazamano wa kipekee kuhusu watu na habari za eneo la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia posti zetu zilizo bora zilizoandikwa kwa lugha ya Kiingereza kwa mwaka 2012. Hii ni zawadi sahihi kabisa ya kuukaribisha mwaka mpya.

Ethiopia: Maandamano ya Waislamu Yashika Kasi

  21 Julai 2012

Jeshi la Polisi nchini Ethiopia waliamua kutumia nguvu kupambana na wanaharakati wa ki-Islamu, likituhumiwa kufanya vitendo haramu katika maeneo yanayochukuliwa kuwa matakatifu katika misikiti, kwa mujibu wa habari zilizoandikwa na ukurasa wa kikundi cha waislam katika mtandao wa Facebook uitwao Dimtsachin Yisema (Iache Sauti Yetu Isikike). Tangu mwezi Mei, Wa-Islamu wa ki-Ethiopia wamekuwa wakiandamana kupinga serikali kuingilia mambo yao ya kidini.

Ethiopia: Ardhi, Historia na Haki katika Eneo la Gambella

  12 Juni 2012

Wanaharakati wa masuala ya ardhi wanatumia hati ya malalamiko ya mtandao, mtandao wa facebook na twita kufanya kampeni dhidi ya unyang’anyi wa ardhi nchini Ethiopia. Inaarifiwa kwamba wanakijiji kwenye jimbo msikini zaidi nchini humo, Gambella, wanalazimishwa kuhamia kwenye vijiji vilivyobuniwa na serikali ili kuwapisha wanaoitwa 'wawekezaji' wakubwa.

Africa: Waafrika Wasimulia Kumbukumbu Zao za Utotoni

  9 Septemba 2010

That African Girl ni blogu yenye mfululizo wa makala zilizoandikwa na Waafrika kutoka dunia nzima kuhusu maisha ya utotoni. Ni blogu inayoelezea kuhusu makuzi katika familia za Kiafrika na uzoefu wa kuishi katika tamaduni mbili.