Habari kuhusu Ethiopia
Waethiopia Waadhimisha Siku ya Wajinga kwa Kuikejeli Televisheni ya Taifa
"Katika kujibu shutuma za wanaharakati hao siku hiyo, #ETv walitangaza kuwa hii [siku ya wajinga] ndio siku pekee ambayo hawaimiliki"
Utani Mitandaoni: Siku ya Wajinga Nchini Ethiopia
Wa-Ethiopia kwenye mtandao wa twita wanasherehekea siku ya wajinga duniani kwa kutangaza habari bandia ambazo zinaiga uongo unaotangazwa na vyombo vya habari vya serikali. Raia mmoja wa Ethiopia anayetwiti: “Wanatangaza uongo wa mchana siku 365 za mwaka, ngoja twarudishie dozi ya kuwatosha yenye habari za uongo kadri tunavyoweza”. Wafuatilie ili...
Mwandishi wa Habari wa Ethiopia Reeyot Alemu Amefungwa Jela kwa Siku 1,000
Mnmo Machi 16, 2014, mwandishi wa Ethiopia anayetumikia kifungo jela Reeyot Alemu amemaliza siku yake ya 1,000 akiwa gerezani. Watumiaji wa mtandao wa Twita walionyesha mshikamano naye kwa kutumia alama habari ya #ReeyotAlemu.
Ethiopia: Mwanablogu Ahukumiwa Miaka 18 Jela kwa “Kuvunja Katiba”
Mnamo Mei 1, Mahakama Kuu ya Ethiopia ilitoa hukumu kali kwa mwandishi aliyeshinda tuzo Eskinder Nega, ambaye sasa atatumikia kifungo cha miaka 18 jela. Mohamed Keita wa Kamati ya Kuwalinda Waandishi anasema, “Kushitakiwa na hatimaye kutiwa hatiani kwa Eskinder na waandishi wengine ni dalili za utawala unaoogopa maoni ya raia wake.”
Kitabu-pepe Kipya cha GV: Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko
"Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko", kinakupa mtazamano wa kipekee kuhusu watu na habari za eneo la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia posti zetu zilizo bora zilizoandikwa kwa lugha ya Kiingereza kwa mwaka 2012. Hii ni zawadi sahihi kabisa ya kuukaribisha mwaka mpya.
Tanzania, Ethiopia: Meles Zenawi ‘Atuma Twiti’ Kutoka Kilindi cha Kaburi
"@zittokabwe tafadhali uwe bora kuliko mimi nilivyokuwa. Huku juu hakuna utani, tayari ninalipia makosa yangu." Twiti iliyotumwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi baada ya kifo chake kwenda kwa Mbunge wa Tanzania Zitto Kabwe na kuibua mjadala mtandaoni.
Ethiopia: Maandamano ya Waislamu Yashika Kasi
Jeshi la Polisi nchini Ethiopia waliamua kutumia nguvu kupambana na wanaharakati wa ki-Islamu, likituhumiwa kufanya vitendo haramu katika maeneo yanayochukuliwa kuwa matakatifu katika misikiti, kwa mujibu wa habari zilizoandikwa na ukurasa wa kikundi cha waislam katika mtandao wa Facebook uitwao Dimtsachin Yisema (Iache Sauti Yetu Isikike). Tangu mwezi Mei, Wa-Islamu wa ki-Ethiopia wamekuwa wakiandamana kupinga serikali kuingilia mambo yao ya kidini.
Ethiopia: Ardhi, Historia na Haki katika Eneo la Gambella
Wanaharakati wa masuala ya ardhi wanatumia hati ya malalamiko ya mtandao, mtandao wa facebook na twita kufanya kampeni dhidi ya unyang’anyi wa ardhi nchini Ethiopia. Inaarifiwa kwamba wanakijiji kwenye jimbo msikini zaidi nchini humo, Gambella, wanalazimishwa kuhamia kwenye vijiji vilivyobuniwa na serikali ili kuwapisha wanaoitwa 'wawekezaji' wakubwa.
Africa: Waafrika Wasimulia Kumbukumbu Zao za Utotoni
That African Girl ni blogu yenye mfululizo wa makala zilizoandikwa na Waafrika kutoka dunia nzima kuhusu maisha ya utotoni. Ni blogu inayoelezea kuhusu makuzi katika familia za Kiafrika na uzoefu wa kuishi katika tamaduni mbili.
Ethiopia: Wanablogu walitetea Shirika la Ndege la Ethiopia baada ya ajali ya ndege
Wanablogu waishio Ethiopia wameharakia kuitetea rekodi ya usalama wa safari za ndege za nchi hiyo siku ya Jumatatu baada ya ndege moja kuanguka karibu na Beirut, ikihofiwa kupoteza maisha ya watu wote 90 waliokuwepo.