Habari kuhusu Kenya kutoka Juni, 2012
Umuhimu wa Kongamano La Sauti za Dunia (Global Voices Summit) hapa Nairobi
Kuanzia tarehe mbili mwezi wa Julai hadi tarehe nne mwezi huo huo, familia ya Sauti za Dunia (Global Voices, GV) pamoja na washiriki wao wa kimataifa, raia wapendao vyombo vya habari na watazamaji watakusanyika pamoja katika hoteli ya Pride-Inn mjini Nairobi kwa kongamano la GV. Bila shaka tukio hili ni la kusisimua na ambalo limekuwa likitarajiwa na wengi kwa shauku kuu.
Kenya: Kilimo cha Bustani Mijini Chashika Kasi
Nchini Kenya, wakazi wa mjijini wanajifunza mbinu mbalimbali za kulima mazao ya chakula kwa ajili ya matumizi binafzi na kwa ajili ya kuuza katika maeneo madogo. kwa watu wenye kipato kidogo au wasio na kipato, ukulima wa mijini unaweza kuwa ndiyo ufumbuzi wa kujihakikishia uwepo wa chakula. Video hizi zinaonyesha jinsi ambavyo chakula kinaweza kuzalishwa katika makasha na vifaa vingine vya kubebea kwa kutumia maeneo na rasilimali kidogo.
Kenya: Intani walipwe au wasilipwe?
Mada hapa ni kuhusu kama inafaaa au haifai kwa intani kulipwa,mjadala ulioanzishwa na @RobertAlai.
Kenya: Wanaharakati wapigana vita dhidi ya ufisadi kwa intaneti
I Paid a Bribe ni njia mojawapo inayotumiwa na wanaharakati dhidi ya ufisadi nchini, kwa kutumia teknolojia mpya ili kuwawezesha kupata ripoti za utoaji wa hongo.' I paid a Bribe' imefuatia muundo wa ‘India Anti-Corruption Portal (IPAB)' na ni ushirkiano kati ya IPAB na Wamani Trust ya Kenya ili kuleta IPAB katika Afrika Mashariki na Kati.
Kenya: Habari za Mlipuko Jijini Nairobi Zatawala Mijadala ya Twita
Kufuatia mlipuko mkubwa ulioathiri vibaya mtaa mkubwa wa Nairobi, Moi Avenue, wakenya na marafiki wa Kenya walitumia mtandao wa twita kuhabarishana, na kusambaza taarifa, kushauriana na kujadili tukio hilo baya.