Habari kuhusu Kenya kutoka Julai, 2009
Kenya: Ukame Uliokithiri Wachochea Mgogoro kati ya Binadamu na Wanyama Pori
Kenya inakabiliwa na ukame mbaya zaidi katika kipindi cha zaidi ya muongo mmoja kwa mujibu wa Idara ya Hali ya Hewa. Ukame huu umeathiri nchi nzima, lakini athari zake zimeonekana zaidi katika jamii ya Kimasai ambayo chanzo zhake cha kwanza cha maisha ni mifugo. Wakikabiliwa na hatari ya kupoteza mifugo...
Afrika: Ujio wa Mkonga wa Seacom Wazua Mjadala
Ujio wa mkonga unaopita chini ya bahari utakao ongeza uwezo na kupunguza gharama za intaneti barani Afrika umewasha majadiliano na mvuto katika ulimwengu wa blogu wa Afrika. Seacom, ambayo inaunganisha Afrika Kusini, Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji na Ulaya pamoja na Asia, ilianza kutumika moja kwa moja Alhamisi, kwa kuziunganisha nchi za Afrika ya mashariki na Afrika ya kusini kwenye mtandao wa dunia wenye wigo mpana.
Afrika: Obama Atumia Nyenzo Mpya za Habari Kuzungumza na Waafrika
“Umeshawahi kutaka kumuuliza kijana wetu wa Nyangoma maswali yoyote? Kwa maneno mengine, je ungependa Rais wa Marekani, Barack Obama ajibu maswali yako?,” ndivyo inavyoanza makala kwenye blogu ya Hot Secrets inayohusu matumizi ya Obama ya zana mpya za habari ili kukutana na kuongea na Waafrika wa kawaida.
Afrika: Wanablogu wamwombolezea Michael Jackson
Barani Afrika, wanablogu wanatoa heshima zao za mwisho kwa Michael Jackson baada ya kifo chake hivi karibuni kwa kutuma picha, video za muziki, mashairi pamoja na tafakari. “Pumzika Kwa Amani” anaandika Mwanablogu wa Kenya WildeYearnings. “Sasa unalo anga zima kucheza kwa madaha kwa staili ya kutembea mwezini…”