Habari kuhusu Harakati za Mtandaoni kutoka Novemba, 2009
Brazil: Mtazamo wa Wakazi wa Vitongoji Maskini
Katika makala hii, tunasikia mitazamo ya wanahabari raia kutoka mradi wa Viva Favela kuhusiana ya vurugu inayotokana na mihadarati huko Rio de Janeiro na jinsi inavyofagia makazi ya walalahoi, kama wanavyoiona mbele ya milango ya nyumba zao.
Azerbaijan: Baada ya Hukumu ya Wanablogu wa Video
Siku chache baada ya hukumu ya vijana wanaharakati wawili wa blogu za video huko Azerbaijan, wanablogu wengine wanaanza kuongea kwa sauti juu ya kifungo cha Adnan Hajizade na Emin Milli....
Ofisa Aweka Wazi Ufisadi wa Polisi kupitia Mtandao
Mnamo tarehe 6 Novemba, afisa wa polisi katika Idara ya Mambo ya Ndani huko Novorossiysk alitumia tovuti yake binafsi kuwasiliana na Waziri Mkuu Vladimir Putin na kuzungumzia matatizo lukuki yanayowakabili maafisa wa polisi nchini Urusi.
Vijana wa Kiyahudi na Kipalestina Watumia Video Kuuelewa Mgogoro
Mashirika mawili tofauti nchini Israel na katika Majimbo ya Palestina yanatumia zana za video ili kuwasaidia vijana wa Kiarabu na Kiyahudi kuuelewa mgogoro na kujenga daraja kati yao.
Cuba: Ukweli wa Sanchez Kutiwa Mbaroni Waibuka
Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika...
Yoani Sanchez Pamoja na Wanablogu Wengine wa Cuba Wakamatwa na Kupigwa
Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú iliweka kiungo kuelekea makala iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na...
Tunisia: Mwanablogu Fatma Arabicca Awekwa Kizuizini
Mwanablogu wa Kitunisia Fatma Riahi ambaye hublogu kama Fatma Arabicca, ameshtakiwa kwa udhalilishaji katika blogu yake na hivi sasa amewekwa kizuizini.Kundi limeundwa kwenye Facebook kumuunga mkono mwanablogu huyu mwenye umri...
Irani: Vuguvugu la Kijani Laupinga Utawala Tena
Upande wa upinzani wa Vuguvugu la Kijani nchini Irani mnamo tarehe 4 Novemba uliendesha maandamano makubwa ambapo maandamano hayo yalikabiliwa na matumizi makubwa ya nguvu ya kuyazuia yaliyofanywa na vikosi vya usalma. Kama ambavyo sasa inatarajiwa, uandishi wa habari wa kiraia nchini Irani haukukosa kitu kwani ulirekodi 'historia' hiyo kupitia simu zao za mikononi.
Kutambulisha Sauti Zinazotishwa
Leo, kitengo cha utetezi cha Global Voices, kinazindua tovuti mpya inayoitwa Threatened Voices, yaani, Sauti Zinazotishwa ili kusaidia kufuatilia unyamazishaji wa uhuru wa kujieleza wa mtandaoni. Inaonyesha ramani ya dunia na mwingiliano wa saa unaosaidia kuonyesha taarifa za vitisho na ukamataji unaofanywa dhidi ya wanablogu duniani kote, na ni mhimili mkuu wa kukusanyia taarifa kutoka katika asasi na wanaharakati walioamua kujitoa muhanga kwelikweli.
Misri: Watu 10 Wenye Ushawishi Zaidi Nchini
Mtoto wa Rais wa Misri, Hosni Mubarak, anayitwa Gamal Mubarak, -- na ambaye anatarajiwa kumrithi baba yake nafasi hiyo -- aliibuka kama mmoja wa washindi 100 wa TIME. Wanablogu wa Ki-Misri wana ya kueleza kuhusu jambo hili.