Habari kuhusu Harakati za Mtandaoni kutoka Januari, 2010
Misri: wanablogu Watiwa Mbaroni Kufuatia Kutembelea kwao Naha Hammady
Leo Misri iliwatia mbaroni wanablogu 20 waliokuwa wakitembelea eneo la Naga Hammady huko Misri ya Juu ili kutoa heshima zao kwa watu waliouwawa katika shambulio la kidini mnano January 7 mwaka huu. Watu 7 waliuwawa kwa risasi huku wengine wengi wakijeruhiwa pale mwuaji alipowamiminia risasi Wakristo wa Madhehebu ya Kikopti waliokuwa wakitoka kanisani mara baada ya Misa ya Krismas (Wakopti husherehekea Krismas kila tarehe 7 Januari). Uamuzi wa kutembelea eneo hilo uliofanywa na wanablogu hao ulikuwa ni kwa lengo la kuungana dhidi ya uhasama wa kidini.
Slovakia, Hungaria: Heri ya Mwaka Mpya!
Uhusiano kati ya nchi mbili jirani za Slovakia na Hungaria ulianza kutetereka katika mwaka uliopita - lakini baadhi ya wananchi wa Slovakia na Hungaria wanafanya juhudi kurekebisha hali hiyo kwa kuzindua kampeni ya mtandaoni inayojulikana kama "Štastný nový rok, Slovensko! / Boldog Új Évet Magyarország!" ("Heri ya Mwaka Mpya, Slovakia!/Heri ya Mwaka Mpya, Hungaria!).
Japan: Tangaza Ujumbe, Tafsiri
Mahojiano ya video [en] ya Kyo Kageura, mkuu wa mradi wa Minna no Honyaku (みんなの翻訳, Tafsiri kwa Wote) [ja], jukwaa jipya la tafsiri ambalo linazisaidia Asasi Zisizo za Kiserikali na...