Habari kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

DRC Kongo: Misuguano Kati ya Kinshasa na Paris Mkutano Unapoanza

  15 Oktoba 2012

Le Potentiel anaandika kwamba [fr] tathmini ya Uvunjaji wa Haki za Binadamu nchini DRC Kongo iliyofanywa na Rais wa Ufaransa Hollande haikuchukuliwa kijuu juu na serikali ya Kongo wakati ambapo Mkutano wa nchi zizungumzazo Kifaransa ndio kwanza umeanza mjini Kinshasa, DRC. SErikali hizi mbili zinaonekana kutofautiana sana kuhusu mambo kama...

Mabadiliko ya Mfumo wa Ustawi wa Jamii ya Kiafrika

  17 Juni 2012

Utekelezaji wa mifumo ya hifadhi ya jamii ya taifa bado uko katika hatua za mabadiliko katika nchi nyingi za Afrika. Mafanikio ya mifumo iliyopo yanajadiliwa na wataalamu wa hifadhi za jamii katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara.

Dondoo za Video: Maandamano, Chaguzi, Utamaduni na GV

  31 Disemba 2011

Baadhi ya habari za kuvutia za Global Voices na video za hivi karibuni kutoka Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, Mashariki na Ulaya Kati, Karibeani pamoja na Marekani ya Kusini, zimeletwa na Juliana Rincón Parra.

Mapinduzi Nchini Niger: Wanablogu Wapumua Pumzi ya Ahueni

  23 Februari 2010

Alhamisi Februari 18 mapinduzi ya kijeshi yalifanyika nchini Niger ambayo kwayo Rais Mamadou Tandja alikamatwa baada ya mapambano ya bunduki katika mji mkuu, Niamey. Miezi michache iliyopita Tandja alibadilisha katiba kinyume cha sheria ili ajiruhusu kuongoza kwa muhula wa tatu katika kile ambacho kilionekana kama dhuluma ya halaiki kwenye kura maoni. Wanablogu wanatoa mitazamo yao juu ya maendeleo haya mapya.

Angola: Ebola Inapokaribia, Mipaka yafungwa

  18 Januari 2009

Baada ya kuzuka kwa ugonjwa wa ebola kwenye Jamburi ya Kidemokrasi ya Kongo, maambukizi ya ugonjwa huo bado hayajafika nchini Angola. Ili kuuzuia kusambaa kwa virusi hatari vya ugonjwa huo, nchi hiyo jirani imefunga mpaka wake na Jamhuri ya Kidemorasi ya Kongo, kadhalika imezuia uhamiaji wa watu kati ya nchi hizo mbili. Anaandika Clara Onofre.

Kivu Mpaka Gaza: Namna Vyombo Vya Habari Vinavyochagua Vipaumbele

  11 Januari 2009

Mdahalo unaodadisi ni kwa nini vita katika Mashariki ya Kongo vinapewa kipaumbele kidogo ikilinganishwa na migogoro inayotokea Mashariki ya kati. Mwandishi wa habari wa Rue89 anauliza, "ikiwa kifo cha Muisraeli mmoja ni sawa na vifo kadhaa vya Wapalestina, ni maiti ngapi za watu wa Kongo zitakazowekwa kwenye mnara wa mazishi huko Gaza?" Wanablogu wa pande zote mbili wanalichambua swala hilo.

Kongo: Utata Watawala Goma

  2 Novemba 2008

Miezi miwili iliyopita mapigano yamezuka tena katika jimbo la mashariki la Kivu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kati ya kundi la upinzani linaloongozwa na Jenerali laurtent Nkunda na majeshi ya serikali, kinyume na makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwezi januari. Mapambano hayo yameongezeka zaidi katika siku 6 zilizopita na, japokuwa usitishaji wa vita hivyo ulitangazwa, hali bado ni ya kutananisha mjini Goma. Yafuatayo ni maoni kutoka kwa wanablogu walioko sehemu hiyo.

Mwangwi wa Sakata la Maziwa China katika Afrika

  1 Oktoba 2008

Nchini China inakadiriwa kuwa watoto 13,000 wameugua tangu sakata la maziwa yasiyofaa kuibuka. Ushawishi na nguvu za China vimeongezeka Afrika, kama ulivyoongezeka uagizwaji wa bidhaa za kila namna, kuanzia viatu vya mazoezi mpaka chakula aina ya tambi. Mabloga hata wale walio mbali kama Kongo au Senegal, wanaguswa na usalama wa bidhaa za kutoka China katika nchi zao, na wanafuatilias habari hiyo (ya maziwa yasiyofaa).