Habari kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Congo (DRC): Video zasaidia kumtia hatiani Thomas Lubanga kwa uhalifu wa kivita

Mnamo tarehe 14, Machi, mahakama ya kimataifa ya makosa ya kivita ilimtia hatiani Thomas Lubanga, kiongozi wa zamani wa waasi Kongo (DRC) Mashariki, kwa kosa la kuwatumia watoto katika vita. Jaji alisema picha za video zilizoonyesha mahojiano na askari hao watoto ziliziongeza uzito wa ushahidi ulioisaidia mahakama kutoa hukumu.

8 Aprili 2012

Mapinduzi Nchini Niger: Wanablogu Wapumua Pumzi ya Ahueni

Alhamisi Februari 18 mapinduzi ya kijeshi yalifanyika nchini Niger ambayo kwayo Rais Mamadou Tandja alikamatwa baada ya mapambano ya bunduki katika mji mkuu, Niamey. Miezi michache iliyopita Tandja alibadilisha katiba kinyume cha sheria ili ajiruhusu kuongoza kwa muhula wa tatu katika kile ambacho kilionekana kama dhuluma ya halaiki kwenye kura maoni. Wanablogu wanatoa mitazamo yao juu ya maendeleo haya mapya.

23 Februari 2010

Angola: Ebola Inapokaribia, Mipaka yafungwa

Baada ya kuzuka kwa ugonjwa wa ebola kwenye Jamburi ya Kidemokrasi ya Kongo, maambukizi ya ugonjwa huo bado hayajafika nchini Angola. Ili kuuzuia kusambaa kwa virusi hatari vya ugonjwa huo, nchi hiyo jirani imefunga mpaka wake na Jamhuri ya Kidemorasi ya Kongo, kadhalika imezuia uhamiaji wa watu kati ya nchi hizo mbili. Anaandika Clara Onofre.

18 Januari 2009

Kivu Mpaka Gaza: Namna Vyombo Vya Habari Vinavyochagua Vipaumbele

Mdahalo unaodadisi ni kwa nini vita katika Mashariki ya Kongo vinapewa kipaumbele kidogo ikilinganishwa na migogoro inayotokea Mashariki ya kati. Mwandishi wa habari wa Rue89 anauliza, "ikiwa kifo cha Muisraeli mmoja ni sawa na vifo kadhaa vya Wapalestina, ni maiti ngapi za watu wa Kongo zitakazowekwa kwenye mnara wa mazishi huko Gaza?" Wanablogu wa pande zote mbili wanalichambua swala hilo.

11 Januari 2009

Kongo: Utata Watawala Goma

Miezi miwili iliyopita mapigano yamezuka tena katika jimbo la mashariki la Kivu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kati ya kundi la upinzani linaloongozwa na Jenerali laurtent Nkunda na majeshi ya serikali, kinyume na makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwezi januari. Mapambano hayo yameongezeka zaidi katika siku 6 zilizopita na, japokuwa usitishaji wa vita hivyo ulitangazwa, hali bado ni ya kutananisha mjini Goma. Yafuatayo ni maoni kutoka kwa wanablogu walioko sehemu hiyo.

2 Novemba 2008

Mwangwi wa Sakata la Maziwa China katika Afrika

Nchini China inakadiriwa kuwa watoto 13,000 wameugua tangu sakata la maziwa yasiyofaa kuibuka. Ushawishi na nguvu za China vimeongezeka Afrika, kama ulivyoongezeka uagizwaji wa bidhaa za kila namna, kuanzia viatu vya mazoezi mpaka chakula aina ya tambi. Mabloga hata wale walio mbali kama Kongo au Senegal, wanaguswa na usalama wa bidhaa za kutoka China katika nchi zao, na wanafuatilias habari hiyo (ya maziwa yasiyofaa).

1 Oktoba 2008