Habari kuhusu Siasa kutoka Aprili, 2012
Senegali:Rais Wade Aandamwa Hata Baada ya Kukubali Kushindwa Uchaguzi
Wakati nchi nyingine zikionekana kushangilia "uungwana" wa Bbdoulaye Wade kukubali matokeo nchini Senegali, wanablogu wa nchi hiyo bado wamemkaba koo Wade kwa kuushambulia Urais wake wakikumbushana ghasia za kuelekea uchaguzi, kubinywa kwa uhuru wa habari na mifano mingi ya utawala mbovu.
Tunisia: Miitikio Tofauti Kufuatia Kuingiliwa kwa Barua Pepe za Waziri Mkuu
Mnamo Aprili 8 “Anonymous Tunisia” kikundi kisichotambulisha majina ya wanachama wao nchini Tunisia (ambacho kinadai kuwa na uhusiano na kikundi cha watu “wasiojitambulisha” ) waingiliao mawasiliano ya watu kiliingilia mawasiliano the ya barua pepe ya waziri mkuu wa Tunisia Hamadi Jebali. Vuguvugu hilo lilipewa jina la utani la (“Achana na Tunisia yangu”) ambayo ni sehemu ya kampeni kuu iitwayo “Operesheni Rejeza Tunisia”.
Ghana: Matumizi ya Vyombo vya Habari vya Kiraia katika Uchaguzi wa Mwaka 2012
Wananchi wa Ghana wanajitayarisha kwa ajili ya uchaguzi wa rais na wabunge ambao utafanyika tarehe 7 Disemba 2012, Jumuiya ya wanablogu wa Ghana imezindua mradi wa uanahabari wa kijamii ambao una nia ya kufunza wanaharakati, vikundi vya kisiasa na wanafunzi kutumia zana za uanahabari wa kijamii kwa ajili ya kwa ajili ya kuafuatilia na kuripoti shughuli za uchaguzi.
Misri: Kundi la “Muslim Brotherhood” dhidi ya Baraza la Kijeshi – Waonyesha Sura Halisi?
“Maandamano ya watu milioni ya kudai kung'olewa kwa baraza la Ganzouri" ndivyo kilivyosomeka kichwa cha habari cha gazeti rasmi la Freedom and Justice Party kufuatia matukio yaliouacha umma wa Wamisri wakiwa mdomo wazi. Je, nini kimetokea kiasi cha karibia "mvunjiko mbaya" kati ya Baraza la Kijeshi na chama cha kisiasa kilichokuwa karibu kutwaa madaraka, pande ambazo zilikuwa na uhusiano mzuri?
Zambia: Rais Awakera Raia Waishio Nje
Rais wa Zambia, Michael Sata, amewakasirisha raia wa nchi hiyo wanaoishi ng'ambo baada ya kuwakejeli wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini Botswana na kufifisha matumaini yao ya kuanzishwa kwa uraia wa nchi mbili katika Katiba ya nchi ya hiyo.
Mali: Raia Washtushwa na Mapinduzi ya Kijeshi
Askari walioasi wametangaza kwamba wanatwaa madaraka nchini Mali, baada ya kuwa wameteka nyara kituo cha televisheni ya taifa pamoja na ikulu. Wanadai kwamba serikali ilishindwa kuvipa vikosi vya jeshi la nchi hiyo msaada ili kuwakabili vilivyo wapiganaji wa kabila la Tuareg waliokuwa wakiteka miji ya kaskazini mwa nchi hiyo.
Ukraine: Gereza la Lukyanivska – “Mahali Watu Wanapotendewa kama Wanyama”
Mnamo tarehe 2 Aprili, Televisheni ya Ukraine ya TVi ilirusha filamu iliyotayarishwa na Kostiantyn Usov kuhusu hali ya maisha na jinsi mahabusu wanavyotendewa katika gereza la Kyiv la Lukyanivska, na pia kuhusu kuenea sana kwa rushwa miongoni mwa askari magereza. Kwa uchache, wengi katika wale ambao tayari wametazama video ya Usov walishtushwa sana na yale waliyoyaona.