Habari kuhusu Siasa kutoka Januari, 2010
Eritrea: Utawala Ulio Madarakani Uondelewe Haraka
Kwa mujibu wa Mohammed Hagos, mradi wa demokrasi katika Eritrea unapaswa uanze kwa kuuondoa madarakani utawala uliopo sasa: “Kikwazo kinachowazuia watu wa Eritrea kujieleza ni utawala wa Issayas. Njia ya kuelekea demokrasia kwa hiyo inaanza na kuuondoa utawala wa Issayas haraka iwezekanavyo…”
Colombia: Ugumu wa Kutofautisha Wazuri na Wabaya
Kwa kupitia upigaji video wa kiraia, asasi tofauti nchini Colombia zinatoa mitazamo yao kuhusu uhalifu, unyama na migogoro inayohusisha matumizi ya silaha, ambayo ni vigumu kuwatofautisha watu wazuri kutoka kwa wabaya.
Marekani: Dkt. Martin Luther King, Jr. Akumbukwa
Martin Luther King Jr. alizaliwa tarehe 15 Januari, 1929 na akawa mmoja wa wasemaji na watetezi wakuu wa Harakati za Haki za Kiraia huko Marekani. Nchini Marekani, anaenziwa kwa sikukuu ya taifa, inayoadhimishwa kila mwaka siku ya Jumatatu ya tatu ya mwezi Januari. Leo, wanablogu wengi nchini Marekani wanaadhimisha kumbukumbu yake kwa kuandika makala za kumuenzi, huku wakiungalisha urithi wake wa masuala ya haki za jamii na masuala ya leo, wakionyesha wazi kuwa miaka 42 baada ya kuuwawa kwa King, maneno yake bado yana maana.
Misri: wanablogu Watiwa Mbaroni Kufuatia Kutembelea kwao Naha Hammady
Leo Misri iliwatia mbaroni wanablogu 20 waliokuwa wakitembelea eneo la Naga Hammady huko Misri ya Juu ili kutoa heshima zao kwa watu waliouwawa katika shambulio la kidini mnano January 7 mwaka huu. Watu 7 waliuwawa kwa risasi huku wengine wengi wakijeruhiwa pale mwuaji alipowamiminia risasi Wakristo wa Madhehebu ya Kikopti waliokuwa wakitoka kanisani mara baada ya Misa ya Krismas (Wakopti husherehekea Krismas kila tarehe 7 Januari). Uamuzi wa kutembelea eneo hilo uliofanywa na wanablogu hao ulikuwa ni kwa lengo la kuungana dhidi ya uhasama wa kidini.
Bolivia: Mshindi wa Zamani wa Mashindano ya Urembo Atangazwa Kugombea Ugavana wa Jimbo la Beni
Bolivia Jessica Jordan kuwa mgombea wa kiti cha ugavana kwa tiketi ya Chama Cha Ujamaa (MAS) huko kwenye jimbo la Beni, ambalo kwa kawaida hudhibitiwa na upinzani.
Misri: Mauaji ya Kinyama ya Naga Hammady
Wanablogu wa Misri wanaelezea kustuka kwao na hasira kwa kuuwawa kwa Wakristu wa dhehebu la Koptiki wakati wa mkesha wa sikukuu yao ya krismasi huko Naga hammady, katika Misri ya Juu. Mhalifu asiyejulikana alipiga risasi hovyo hovyo kwenye umati watu baada ya waumini kumaliza maombi na wakiwa wanaelekea majumbani kwao.
Sri Lanka: Kulipia Vyombo Vya Kimataifa Vya Habari kwa Ajili ya Uchaguzi wa Ndani
Kampeni kabambe ya Rais wa Sri Lanka aliye madarakani, Mahinda Rajapakshe inajumuisha manunuzi ya nafasi za matangazo katika tovuti mashuhuri za vyombo vya habari duniani. Groundviews anahoji sababu ya kuvilipa vyombo vya habari vya kimataifa kwa ajili ya uchaguzi wa ndani ya nchi.
China na Hong Kong: Walinzi na Wauaji
Bodyguards and Assassins (Walinzi na Wauaji) ni filamu ya kuchangamsha iliyotolewa wakati wa Krismasi huko China, Hong Kong na Taiwan. Ikiwa ni filamu ya kizalendo, awali ilipangwa kutolewa mwezi Oktoba ili kusherehekea maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Watu wa China lakini ikacheleshwa mpaka mwisho wa mwaka 2009. Tofauti...
Ethiopia: Adhabu ya Kifo Ili Kuwatisha Waethiopia
Berhanu Nega, mmoja kati ya watu waliohukumiwa kifo na mahakama ya Ethiopia anasema hashangazwi na adhabu ya kifo.
Sudani: Je, Umoja Bado Ni Chaguo la Kimkakati
Akiandika kwa Kiarabu, mwanablogu wa Kisudani Ayman Hajj anajadili siasa za nchi yake na kwa nini watu wengi wa Sudani wanapoteza imani katika umoja.