Habari kuhusu Siasa kutoka Agosti, 2010
Tunisia: Picha ‘Zilizochakachuliwa’ ni Dalili ya Hali Halisi katika Vyombo vya Habari vya Kitaifa
Utumiaji vyombo vya habari vya kitaifa nchini Tunisia kama chombo vya kupigia propaganda ni jambo ambalo limeripotiwa vya kutosha. Ushahidi wa hivi karibuni kabisa wa utumiaji mbaya wa vyombo vya habari umewekwa bayana na wanablogu wa nchi hiyo mnamo tarehe 20 Agosti baada ya magazeti ya Le Temps na Assabah kuchapisha ripoti kuhusu taasisi ya hisani ya Zeitouna kutuma msaada wa kibinadamu wa chakula kwa waathirika wa mafuriko nchini Pakistani.
Cape Verde: Midahalo Kuhusu Vijana na Siasa Inayoendelea Huko Ureno
Kuna kundi la raia wa Cape Verde ambalo huandaa mikutano mjini Lisbon ili kujadili uhusiano kati ya vijana na siasa, kama anavyoeleza Suzano Costa katika video [pt] kama ilivyowekwa tena na Amilcar Tavares. Katika blogu yao – Tertúlia Crioula [pt] – unaweza kusoma maelezo yaliyochukuliwa kutoka “Cape Verde katika Mdahalo” kadhalika unaweza...
Malaysia: Je, Uhuru wa Habari Unaelekea Wapi Sasa?
Picha uliyonayo ni kwamba Malaysia inaweza kuwa ni moja ya nchi zinazokua haraka kiuchumi katika bara la Asia, lakini je unafahamu kuwa ilikuwa katika nchi tatu za mwisho (nchi ya 131) kwenye masuala ya uhuru wa vyombo vya habari? Je wananchi na vyama vya upinzani vinavyopigana dhidi ya uchujwaji wa habari wanapata ahueni? Tutajua ukweli kwa kuangalia hali ya sasa ya uhuru wa vyombo vya habari nchini Malaysia.
Irani: Kampeni ya Kutaka Mwanablogu-Mpiga Picha Hamed Saber Kuachiwa Huru
Zaidi ya wanafunzi 70 waliohitimu elimu ya chuo kikuu na wasomi wa nchini Irani wametoa wito wa kuachiwa kwa Hamed Saber, ambaye ni mwanablogu-mpiga picha na mwanasayansi wa kompyuta wa nchini humo aliyekamatwa pasipo sababu za kuelewekea mnamo tarehe 21 Juni 2010 jijini Tehran.
Afrika Kusini: Wanablogu Wajadili Hukumu ya Mkuu wa Zamani wa Jeshi la Polisi
Siku ya ijumaa tarehe 2 Julai 2010, aliyekuwa mkuu wa polisi na rais wa zamani wa Shirika la Kimataifa la Polisi (Interpol) Jack Selebi alihukumiwa kwa kosa la rushwa. Hukumu hiyo imezua mdahalo nchini na kadhalika imeacha maswali mengi yasiyo na majibu.
Italia: HAPANA kwa Vikwazo Dhidi ya Uhuru wa Kujieleza wa Mtandaoni
Muswada mpya wa habari na Unasaji wa siri wa Mawasiliano ambao umewasilishwa kwenye bunge la Italia unaweza kuanzisha "hatari ya malipo ya fidia" kwa wanablogu wote na vyombo vya habari vya mtandaoni.
Udhibiti Nchini Singapore
Singapore imesababisha kelele kubwa baada ya kupiga marufuku filamu ya aliyewahi kuwa mfungwa wa kisiasa na kumkamata mtunzi Mwingereza wa kitabu kilichoandiaka kuhusu adhabu ya kifo nchini humo. Wanablogu wanajadili.