Wanajeshi waasi wametangaza kwamba wametwaa madaraka nchini Mali , baada ya kukiteka kituo cha televisheni ya taifa pamoja na ikulu ya nchi hiyo.
Wanadai serikali ya Rais Amadou Toumani Touré imeshindwa kutoa ushirikiano kwa vikosi vyake kijeshi katika mapambano dhidi ya waasi wa Tuareg kaskazini mwa nchi hiyo ambao wanataka kujitenga kutoka nchi hiyo.
Raia wengi wamepatwa na mshtuko iweje mapinduzi yafanyike kipindi cha mwezi mmoja tu kabla ya uchaguzi uliokuwa umepangwa kufanyika tarehe 29 Aprili, 2012? Bila shaka kulikuwa na nadharia nyingine za kueleza tukio hilo na hatua hiyo ya kijeshi.
Kapteni Sanogo ndiye kiongozi wa Kamati ya kijeshi ya Taifa ya Kurejesha Demokrasia na Nchi (CNRDR) ambao wanasema wataongoza serikali ya mpito mpaka uchaguzi utakapofanyika.
Msemaji wa kamati hiyo, Lieutenant Kanoré alisema kwamba ingawa wamesimamisha katiba na kuvunja taasisi zilizopo, hawana kusudio la kung’ang’ania madaraka. Mapigano kati ya wanajeshi wanaounga mapinduzi hayo na wale wanaomwunga mkono Rais Toure bado yangali yakiendelea.
Baadhi ya wanasiasa na maafisa wa ngazi za juu wameripotiwa kuwekwa kizuizini mjini Bamako, makao makuu ya nchini hiyo.
http://www.youtube.com/watch?v=EbZeQDA3UDU&feature=youtu.be&a
Raia wengi wa Mali wameshtushwa kwa kiasi kikubwa na mwelekeo wa matukio. Hapa ni baadhi ya miitikio baada ya kufahamu kuwa wanajeshi waasi walikuwa wametwaa madaraka [fr na ing]:
@TheSalifou: J'ai peur pour mon pays…#Mali
@Anniepayep: vraiment! La honte! RT @juliusessoka En Afrique, sortir de l'auberge donne sur les caniveaux. #Mali #PauvrePays
@Abdou_Diarra: Le président malien Amadou Toumani Touré, irait bien et serait « en lieu sûr », selon un militaire loyaliste #Mali
@Youngmalian: #ATT a été élu démocratiquement par le peuple et son mandat se termine en Juin. de quel droit les militaires agissent au nom du peuple #Mali
@ibiriti: demokrasia haimaanishi tu ni mipangilio ya uchaguzi ili kubadili watu wasio na uwezo na kuwaweka wengine. Ni lazima itoe huduma
@philinthe_: Benki na vituo vya mafuta vilifungwa mjini #Bamako #Mali. Ninaongea na madereva teksi wanataka kulipwa mara dufu ya nauli inayofahamika. Kwenda Sotrama bado ni kati ya sarafu za Mali CFA 100-150
@temite: Chochote kitakachotokea, kitakachoathirika hakikosi kuwa ni umoja, umoja wa kidugu baina ya watu na utamaduni #Mali
Mpango wa siri unaonekana wazi kufuatia mapinduzi kufanyika majuma machache tu kabla ya uchaguzi ambao tayari umeshapangwa [fr]:
@diatus2: le coup d'état était prévisible au #mali car ATT laissant durer la rebellion touareg pour avoir un 3e mandat
@Giovannidjossou: #ATT ne faisait rien contre les #terroristes au nord #Mali car ces troubles lui permettaient de repousser les #élections de juin prochain !
@Joe_1789: JE DENONCE: Le coup d'Etat ourdi par des bandits armés, à la solde de la Françafrique, contre le Mali et son président démocratiquement élu.
Ukurasa wa Twita wa Ofisi ya Rais wa Mali haukuwa na taarifa mpya tangu Machi 21 ilipokanusha kuangushwa kwa serikali hiyo [fr]:
@PresidenceMali: Démenti formel : Le Ministre de la Défense n'est ni blessé ni arrêté. Il est à son bureau où il poursuit calmement sa journée de travail