· Machi, 2010

Habari kuhusu Siasa kutoka Machi, 2010

Martinique: Uchaguzi, utata na kugomea uchaguzi

  23 Machi 2010

Jumapili ya tarehe 14 Machi, raia wote wa Ufaransa wakiwemo wale wa idara za ng’ambo za Ufaransa walitakiwa kupiga kura... Lakini michakato miwili ya uchaguzi katika kipindi cha miezi mitatu inaweza kuwachosha 55.55% ya wapiga kura wa Martinique ambo waliamua kubaki majumbani.

Afrika Kusini: Ubaguzi wa Julius Malema

Wakati tabia za Rais Jacob Zuma zimekuwa zikizua mijadala mikali na yenye uhai katika ulimwengu wa blogu wa Afrika Kusini, hivi sasa ni mwanasiasa mwenye utata ambaye pia ni rais wa Umoja wa Vijana wa ANC, Julius malema ambaye anatengeneza vichwa vya habari. Hivi karibuni, aliwaongoza wanafunzi katika kuimba wimbo wa zamani wa kupinga ubaguzi wa rangi unaoitwa Ua Kaburu.

Thailand: Utulivu Kabla ya Kimbunga?

  14 Machi 2010

Maandanmano ya kuipinga serikali ya Machi 12 yalimalika salama huku kundi la Mashati Mekundu likiapa kurejea tena mitaani mwishoni maw juma hili ili kuendelea kushinikiza kuvunjwa kwa bunge na kuitisha uchaguzi mkuu. Wanablogu na watumiaji wa Twita wanatoa maoni yao.

Naijeria: Ghasia Zalipuka Huko Jos Kwa Mara Nyingine

Huko Jos, machafuko yanaelekea kujitokeza katika mizunguko inayozidi kuwa midogo: machafuko mabaya yaliukumba mji huo mwaka 1994, 2001, 2008, na – hata miezi miwili iliyopita – mnamo mwezi Januari 2010. Mgogoro wa sasa unasemekana kuwa ulianza katika tukio la kisasi kilichotokana na uharibifu uliotokea mwezi Januari, na, kama ilivyokuwa kwenye machafuko yaliyopita, mapambano ya sasa huko Jos yamekuwa yakipiginwa katika misingi ya kidini.