Habari kuhusu Siasa kutoka Februari, 2013
Mgomo wa Nchi Nzima Wamshitua Rais wa Malawi
Rais wa Malawi Joyce Banda atupilia mbali shinikizo la kujiuzulu mara baada ya mamia ya maelfu ya wafanyakazi wa umma kuandamana kwa wiki mbili kuishinikiza serikali kuongeza mishahara, hali iliyopelekea kufungwa kwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Malawi na kusababisha hali ya taharuki mahospitalini na mashuleni.
Bulgaria: Gharama Kubwa za Nishati Zasababisha Maandamano
Ruslan Trad anataarifu kuwa, siku ya Jumapili tarehe 17 Februari, makumi ya maelfu ya watu katika mji mkuu wa Bulgaria, Sofia pamoja na majiji mengine waliendelea na maandamano kupinga bei kubwa za nishati ya umeme pamoja na gharama za kupasha joto.
Udhaifu wa Watawala wa Afrika unajionesha Mali?
Ousmane Gueye katika tovuti ya Mondoblog anaandika [fr] kuhusu kuchelewa kupeleka vikosi vya kijeshi kasikazini mwa Mali: Kama tungekuwa tunasaiili matokeo ya watu wenye amani na huru kuingilia kati hali ya mambo nchini Mali, basi ni wazi kuwa kwa kuchelewa kupeleka vikosi vya ulinzi, nchi za Afrika zimewakosea wananchi wa Mali...
Wakati Papa Anajiuzulu, Warusi Wajiuzulu kwa Putin
Pasipokutaka kujua matokeo ya kujiuzulu kwa Papa Benedict na athari yake kwa imani ya Kikatoliki au tafsiri ya hatua hiyo kufuatia kashfa ya udhalilishaji iliyowakabili kwa watawa, RuNet walioweka habari hiyo kwenye safu za vichekesho.