Habari kuhusu Habari za Hivi Punde kutoka Februari, 2010
Chile: Tetemeko Kubwa la Ardhi lenye Ukubwa wa 8.8 Laikumba Chile
Saa 9:34 usiku kwa saa za Chile, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.8 liliukumba mwambao wa eneo la Maule nchini Chile. Tetemeko hilo liliutetemesha mji mkuu wa Santiago uliopo Kilomita 325 kutoka katika kiini cha tetemeko hilo. Uharibifu mkubwa umeripotiwa nchin nzima, na idadi ya waliofariki inazidi kwenda juu.
Nijeria: Baada ya miezi miwili bila uongozi, kaimu Rais mpya
Baada ya wiki za mivutano ya kisiasa, Baraza la Seneti lilimthibitisha Goodluck Jonathan kama kaimu Rais. Wengi kwenye ulimwengu wa blogu waliliona tukio hilo kama sababu ya kusherehekea… lakini wengine waliliona kama jambo la kutia hofu, wakieleza kwamba japokuwa kutwaa madaraka kwa Jonathan kunaweza kuwa ni ulazima wa kisiasa, kutwaa huko hakujaruhusiwa wazi na katiba ya Naijeria.
Ethiopia: Wanablogu walitetea Shirika la Ndege la Ethiopia baada ya ajali ya ndege
Wanablogu waishio Ethiopia wameharakia kuitetea rekodi ya usalama wa safari za ndege za nchi hiyo siku ya Jumatatu baada ya ndege moja kuanguka karibu na Beirut, ikihofiwa kupoteza maisha ya watu wote 90 waliokuwepo.
Mapinduzi Nchini Niger: Wanablogu Wapumua Pumzi ya Ahueni
Alhamisi Februari 18 mapinduzi ya kijeshi yalifanyika nchini Niger ambayo kwayo Rais Mamadou Tandja alikamatwa baada ya mapambano ya bunduki katika mji mkuu, Niamey. Miezi michache iliyopita Tandja alibadilisha katiba kinyume cha sheria ili ajiruhusu kuongoza kwa muhula wa tatu katika kile ambacho kilionekana kama dhuluma ya halaiki kwenye kura maoni. Wanablogu wanatoa mitazamo yao juu ya maendeleo haya mapya.
India: Ugaidi Waikumba Pune
Mnamo majira ya saa 1:30 jioni (Februari 13, 2010) mlipuko wa bomuuliua watu 9 na kuwajeruhi wengine 57 katika mgahawa maarufu kwa watalii uliopo katika mji wa Magharibi wa Pune, India. Hisia ziko juu huku wanablogu na watumiaji wa twita wakitoa maoni.