Habari kuhusu Habari za Hivi Punde kutoka Aprili, 2011
Côte d'Ivoire: Kuanguka kwa Laurent Gbagbo
Laurent Gbagbo alikamatwa katika makazi yake ya Cocody, pamoja na mkewe, Simone, na msafara wa watu wa karibu. Miezi mitano baada ya kukataa kukabidhi madaraka kwa rais anayetambuliwa kimataifa kama rais mpya wa Côte d'Ivoire, Alassane Ouattara, mgogoro nchini humo hivi sasa unaelekea kufikia hitimisho.Mtiririko wa matukio yaliyopelekea kukamatwa kwa Gbagbo yaliorodheshwa kwa kina kwa njia ya video za kwenye mtandao ambazo zilitolewa maoni kwenye mtandao.
Côte d'Ivoire: Abijani kwenye masaa ya kudhoofu kwa utawala wa Gbagbo
Siku mbili zilizopita zimekuwa na utajiri katika misuguano na mivutano nchini Côte d'Ivoire. Vikosi vinavyomtii Ouattara, vilianza mashambulizi kuelekea Kusini na Magharibi mwa nchi hiyo. Katika siku zisizozidi tatu, walifanikiwa kuikamata miji ya Douékoué na kufika Yamoussoukro tarehe 30 Machi. Wa-Ivory wanatoa maoni yao kuhusu wafungwa kutoroka, kufungwa kwa televisheni ya taifa na sehemu aliyo Gbagbo:
Japani: Tsunami yaathiri eneo la pwani, yaacha kila kitu kimeharibiwa
Kufuatia tetemeko kubwa kuwahi kutokea nchini, Japani imekumbwa na tsumani mbaya zaidi iliyowahi kutokea. Watu wengi nchini kote wameganda kwenye luninga zao wakati vipande vya habari vinavyoonesha tsunami lenye urefu wa zaidi ya mita 7 kwenda juu likisomba magari na majengo.
Tetemeko kubwa kuwahi kutokea nchini Japani
Siku ya Ijumaa, Machi 11, 2011 saa 8:46:23 mchana saa za Japani, tetemeko lenye vipimo vya tetemeko 8.9 liliikumba Japani, lilikiwa kubwa kuwahi kuripotiwa katika historia ya Japani.
Côte d'Ivoire: Televisheni ya Taifa RTI Inawezekana kuwa Inatangaza Kutokea Kwenye Gari la Matangazo
Kama vile alivyoelezea Julie Owono , ni vigumu kupembua mapambano ya kudhibiti vyombo vya habari vya Pwani ya Pembe (Cote d'Ivoire). Taarifa kutoka Waandishi Wasio na Mipaka inaashiria kuwa RTI...
Saudi Arabia: Mfalme Awaahidi Wananchi wa Saudia Fedha Zaidi
Fedha zaidi zimeahidiwa kutolewa kwa wananchi wa Saudia, ahadi ambayo Mfalme Abdulla ameitoa kupitia hotuba yake kwa taifa leo. Katika hotuba hiyo iliyokuwa fupi, Mlinzi wa Misikiti Miwili Mitukufu aliwashukuru viongozi wa dini, waandishi na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa juhudi walizofanya kutetea ufalme. Matamko na Amri vilifuata ya kwamba mabilioni yatagawanywa kwa watu wa Saudia.