· Februari, 2009

Habari kuhusu Habari za Hivi Punde kutoka Februari, 2009

Misri: Wanablogu Wafuatilia Milipuko ya Mabomu Mjini Kairo

  26 Februari 2009

Mtalii wa Kifaransa ameuwawa na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya msikiti wa Al Hussein uliopo katika eneo la utalii la Khan Al Khalili mjini Kairo. Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.

Madagaska: Zaidi ya 25 Wauwawa Katika Maandamano Kuelekea Ikulu

  9 Februari 2009

Watu wapatao 25 walipigwa risasi na kuuwawa leo katika mji mkuu wa Madagaska, Antananarivo, wakati wa maandamano ya kuelekea ikulu ya nchi hiyo yaliyoitishwa na meya wa jiji Andry Rajoelina baada ya kujitangaza kama kiongozi wa serikali mpya ya mpito katika mkutano wa hadhara wa kisiasa. Katika majuma yaliyopita, ugombeaji wa nguvu za kisiasa kati ya Meya na Rais Marc Ravolamanana kumesababisha ghasia na uporaji.