Habari kuhusu Habari za Hivi Punde kutoka Septemba, 2010
Colombia: maoni ya Awali Kuhusu Kifo cha Kiongozi wa FARC ‘Mono Jojoy’
Víctor Julio Suárez, ambaye anajulikana zaidi kama Jorge Briceño or Mono Jojoy, mmoja wa viongozi wa juu wa Majeshi ya Ukombozi wa Colombia (FARC), aliuwawa katika kile kilichoitwa "Operesheni Sodoma." Watumiaji wa Twita wa Colombia walianza mara moja kuandika maoni yao kuhusu habari hiyo.
Msumbiji: Maputo katika Hali ya Tahadhari Kutokana na Machafuko
Jiji la Maputo lipo kwenye hali ya tahadhari wakati machafuko yakisambaa kutokana na kupanda kwa bei ya mkate, maji na umeme. Wakazi wanataarifu kuwepo kwa vurugu mitaani huku hali ikizidi kuwa mbaya.