Habari kuhusu Zambia
Zambia 2011: Matukio Mawili Yaliyotikisa Taifa
Matukio mawili nchini Zambia yatatambuliwa kama matukio yaliyoitikisa nchi hiyo mwaka 2011. Tukio la kwanza lilikuwa ni kifo cha Rais wa pili wa Jamhuri Frederick Chiluba na tukio la pili lilikuwa kushindwa kwa chama cha MMD baada ya miaka 20 madarakani.
Zambia: Magari Mapya ya Kifahari ya Mtoto wa Rais Yasababisha Minong’ono
Taarifa zilizotangazwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya Kiraia ya Committee of Citizens, Gregory Chifire, kwamba mtoto wa kiume wa rais wa Zambia, Mulenga Sata, hivi karibuni alijipatia magari mawili ya kifahari, zimevutia hisia mchanganyiko kutoka kwa wa-Zambia watumiao mtandao
Zambia: Rais Sata Aituhumu Benki Kuu Kuchapisha Noti Bandia
Rais Michael Sata ameweka wazi kwamba Benki Kuu ya Zambia kwa maelekezo ya kilichokuwa chama cha Upinzani nchini humo MMD, ilichapisha “noti bandia” ambazo inasemekana ziko kwenye mzunguko wa fedha. Hata hivyo, Chama cha MMD kwa kupitia Waziri wake wa zamani wa Fedha Situmbeko Musokotwane, kimekana tuhuma hizo kikisema Benki Kuu inayo uhuru wa kuchapisha noti mpya za ziada bila kuwasiliana na Waziri wa Fedha ama Rais kwa sababu ina mamlaka kamili ya kufanya hivyo.
Zambia: Furaha ya kufanya Kazi na jamii za Vijijini Huko Zambia
Rakesh Katal anaeleza furaha na changamoto za kufanya kazi na jamii za huko Zambia vijijini.
Upinzani Waongezeka dhidi ya Mapendekezo ya Tanzania na Zambia katika Makubaliano ya CITES
Upinzani unaongezeka dhidi ya mapendekezo ya Zambia na Tanzania ya kuruhusiwa na Makubaliano ya Biashara ya Kimataifa ya Makundi ya Mimea na Wanyama Walio Katika Hatari ya Kutoweka (CITES), kuuza hifadhi ya pembe za ndovu walizonazo.