Habari kuhusu Zambia

Zambia 2011: Matukio Mawili Yaliyotikisa Taifa

  8 Januari 2012

Matukio mawili nchini Zambia yatatambuliwa kama matukio yaliyoitikisa nchi hiyo mwaka 2011. Tukio la kwanza lilikuwa ni kifo cha Rais wa pili wa Jamhuri Frederick Chiluba na tukio la pili lilikuwa kushindwa kwa chama cha MMD baada ya miaka 20 madarakani.

Zambia: Rais Sata Aituhumu Benki Kuu Kuchapisha Noti Bandia

  13 Disemba 2011

Rais Michael Sata ameweka wazi kwamba Benki Kuu ya Zambia kwa maelekezo ya kilichokuwa chama cha Upinzani nchini humo MMD, ilichapisha “noti bandia” ambazo inasemekana ziko kwenye mzunguko wa fedha. Hata hivyo, Chama cha MMD kwa kupitia Waziri wake wa zamani wa Fedha Situmbeko Musokotwane, kimekana tuhuma hizo kikisema Benki Kuu inayo uhuru wa kuchapisha noti mpya za ziada bila kuwasiliana na Waziri wa Fedha ama Rais kwa sababu ina mamlaka kamili ya kufanya hivyo.