Habari kuhusu Zambia

Kitabu-pepe Kipya cha GV: Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko

  30 Disemba 2012

"Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko",  kinakupa mtazamano wa kipekee kuhusu watu na habari za eneo la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia posti zetu zilizo bora zilizoandikwa kwa lugha ya Kiingereza kwa mwaka 2012. Hii ni zawadi sahihi kabisa ya kuukaribisha mwaka mpya.

Kupigia Kura Maajabu Saba ya Dunia barani Afrika

  27 Disemba 2012

Shindano la kila mwaka limezinduliwa kwa ajili ya watu kupiga kura kuchagua maajabu saba yaliyo bora zaidi barani Afrika. Na tayari upigaji kura umeshaanza. Baadhi ya maajabu ya asili yaliondolewa katika orodha ya mwisho ya kupigiwa kura na hivyo baadhi ya wanablogu waliongeza mapendekezo yao katika blogu zao. Tazama baadhi ya picha hapa:

Zambia: Filamu yaYouTube Kuhusu Athari za Machimbo ya Madini

  15 Oktoba 2012

Filamu ya Uchunguzi yenye jina "Zambia: Shaba Nzuri, Shaba Mbaya" inayohusu machimbo ya shaba nchini Zambia na athari zake kwa jamii imewekwa kwenye mtandao wa YouTube na mpaka sasa imevuta watazamaji zaidi ya 6,000. Baada ya kuitazama filamu hiyo, mtumiaji mmoja wa mtandao wa YouTube aliandika, "Jililie eeh nchi yangu nzuriKwa nini tubaki masikini katikati ya utajiri huu wa madini yanayochimbwa kwa gharama ya afya za wenyeji?"

Kocha wa Timu ya Taifa ya Zambia Atunukiwa Ukaazi wa Kudumu

  30 Agosti 2012

Zambia imewahi kuwa na makocha wengi wa kigeni wa timu ya Taifa ya soka, lakini ni Mfaransa Herve Renard, aliyeongoza timu hiyo hadi kushina Kombe la Washindi Barani Afrika mwaka 2012, aliyepata upendeleo wa pekee. Ili kutambua mafanikio yake haya, serikali imemtunuku ukaazi wa kudumu lakini uamuzi huo unaonekana kuwekewa chumvi ya kisiasa.

Zambia: Maoni na Hisia Tofauti baada ya Mwakilishi Kutolewa kwenye Mashindano ya Big Brother

  31 Mei 2012

Kuondolewa kwa mwakilishi wa Zambia, mwanamuziki anayefahamika zaidi kwa jina la Mampi, kutoka katika mashindano yanayoendelea ya Big Brother Africa, kumepokelewa kwa hisia na maoni tofauti miongoni mwa watumiaji wa mtandao. Big Brother Africa: StarGame ni toleo la saba la mfululizo wa mashindano hayo maarufu zaidi barani Afrika yanayoonyesha moja kwa moja kupitia televisheni maisha ya washiriki.

Zambia: Rais Awakera Raia Waishio Nje

  15 Aprili 2012

Rais wa Zambia, Michael Sata, amewakasirisha raia wa nchi hiyo wanaoishi ng'ambo baada ya kuwakejeli wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini Botswana na kufifisha matumaini yao ya kuanzishwa kwa uraia wa nchi mbili katika Katiba ya nchi ya hiyo.

Zambia: Kiongozi wa Upinzani Awa wa Kwanza Kulihutubia Bunge la Facebook

  25 Januari 2012

Rais wa Chama cha upinzani cha NAREP (National Restoration Party) Elias Chipimo Jr. amekuwa mwanasiasa wa kwanza katika nchi hiyo “kulihutubia” bunge la Facebook nchini Zambia linaloaminika kuwa na wanachama 1,318 baada ya kuruhusiwa na “Spika” kutuma ujumbe wake wa mwisho wa mwaka.