Habari kuhusu Kiingereza kutoka Machi, 2010
Serikali ya Japani: Kuhusu Kuanguka kwa Mfumo wa Ajira
Chombo kinachotumika kufanya tafakari nzito cha Baraza la Mawaziri la Japani, Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (内閣府 経済社会総合研究所)(ESRI) kimechapisha matokeo ya utafiti yaliyopima hadhi ya sasa ya ajira ya maisha na ulipaji ujira kwa kutumia cheo cha mtu (yaani, mfumo wa ajira wa Kijapani). Walitumia data (1989 –...
Siku ya Ada Lovelace: Kuwapongeza Wanawake Wanajishughulisha Kupigania Teknolojia na Uwazi Ulimwenguni
Katika kusherehekea Siku ya Ada Lovelace tunawaletea makala fupifupi kuhusu wanawake kadhaa walio sehemu mbalimbali duniani ambao hutumia teknolojia ili kuzifanya serikali ziwe wazi na zinazowajibika zaidi.
Global Pulse 2010: Mwaliko wa kuzungumza na watoa uamuzi mtandaoni
Kuanzia tarehe 29 hadi 31 Machi, vuguvugu linalojulikana kama Global Pulse 2010, yaani Mapigo ya Moyo ya Ulimwengu 2010, linakusudia kuwakusanya jumla ya watu 20,000 kupitia mtandao ili wafanya mazungumzo kuhusu mada mbalimbali kuanzia zinazohusu maendeleo ya binadamu hadi sayansi na teknolojia.
China: Uchi Ulio Rasmi
Serikali moja ya mji huko katika Jimbo la Sichuan sasa inaitwa “Serikali ya Kwanza nchini China Iliyo Uchi kabisa” baada ya kuwa maafisa wa mji huo kuweka mishahara na matumizi ya serikali kwenye tovuti. Kutajwa kwa suala la ‘uchi au utupu’ katika machapisho mengi ya Kichina katika siku za karibuni...
Pakistani: Vitendo vya Unyanyasaji Watoto Vyaongezeka
Msemo 'Unyanyasaji watoto' hutumika kueleza vitendo vya aina mbalimbali vilivyo jinai na vinavyofanywa dhidi ya watoto. Wanablogu wanajadili vitendo hivi vya unyanyasiaji watoto vinavyokera na vinavyozidi kuongezeka nchini Pakistani.
Ghana: tamasha la Twestival 2010 Mjini Accra: Shughuli Yenye Maana?
Kama uanahabari wa kijamii unabadilisha mtindo ya mawasiliano katika nchi za Magharibi, basi kwa hakika haujapungukiwa katika kufikia sehemu zinazovutia barani Afrika. . Kwa hiyo haishangazi kwamba MacJordan, wa Global Voices, anashirikiana na Rodney Quarcoo ili kulifikisha tukio hili la kuburudisha kwa watu wa Ghana.
Martinique: Uchaguzi, utata na kugomea uchaguzi
Jumapili ya tarehe 14 Machi, raia wote wa Ufaransa wakiwemo wale wa idara za ng’ambo za Ufaransa walitakiwa kupiga kura... Lakini michakato miwili ya uchaguzi katika kipindi cha miezi mitatu inaweza kuwachosha 55.55% ya wapiga kura wa Martinique ambo waliamua kubaki majumbani.
Mali: Vitambaa Vyasuka Nguzo za Uchumi na Utamaduni
Kwa kupitia video, tunaona na kujifunza kuhusu umuhimu wa utamaduni na ongezeko la kiuchumi ambalo utengenezaji vitambaa huwapa baadhi ya watu na mashirika nchini Mali. Vikundi vya wanawake, wasanii na watalii wote wananufaika na utamaduni huu wa kutia rangi vitambaa na upakaji rangi kwa kutumia matope.
Lebanoni: Wafanyakazi wa Ndani Wanaotoroka
“Mfanyakazi wa ndani anapotoroka kutoka kwenye nyumba ya mwajiri wake, kituo cha polisi hakiwezi kufanya lolote kwa sababu hakuna sheria dhidi ya wafanyakazi wa ndani wanaotoroka. Kwa hiyo ofisa wa kituo cha polisi anamwambia mwajiri wa ki-Lebanoni aseme kuwa (mtoro huyo) aliiba pesa,” anaandika Ethiopian Suicides.
Uganda: Wanafunzi Wacharuka, Kampala Yawaka Moto
Jumanne, majanga mawili tofauti yaliikumba Kampala, mji mkuu wa Uganda: wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Makerere walifanya ghasia baada ya wanafunzi wenzao wawili kupigwa risasi. Na makaburi ya Kasubi, ambayo ni sehemu ya Urithi wa Dunia ya UNESCO na eneo la kaburi la mfalme wa moja ya makabila makubwa zaidi ya Uganda, liliteketea kwa moto.