Habari kuhusu Kiingereza kutoka Julai, 2013
Hali ya Uislamu Katika Asia ya Kusini
Murray Hunter wa Chuo Kikuu cha Malaysia Perlis anajadili hali ya jamii ya Kiislamu katika Asia ya Kusini pamoja na masuala yanayohusiana na kukua kwa Uislamu katika eneo hilo. Umaskini, kujua kusoma na kuandika, elimu, kuhamishwa, ukabaila, ukosefu wa ajira, ukandamizaji, na udhibiti ni mambo yanayowaonea Waislamu ndani ya ASEAN. Serikali pamoja na...
Tamko la Kurekebisha Sheria Zinazokwaza Uhuru wa Vyombo vya Habari Nchini Vietnam
Zaidi ya wanablogu 60 wa Ki-vietinam walitia saini tamko la pamoja kuitaka serikali ya Vietnam kuboresha rekodi ya haki za binadamu na ahadi wanapowania uanachama katika Baraza la Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu: Serikali ya Vietnam pia inahitaji kutathmini hali ya haki za binadamu katika nchi hiyo na wa-Vietinamu pia wana haki ya...
Barua ya Wazi ya Kushinikiza Kuachiwa Huru kwa Mwanasheria
Mnamo Julai 23, 2013, zaidi ya raia 400 wa China wamesaini barua ya kushinikiza serikali ya China kumuachia huru Xu Zhiyong, ambaye ni mwanasheria mashuhuri na mpigania haki aliyekamatwa mnamo Julai 16 baada ya kushinikiza kuachiwa kwa wanaharakati pamoja na kuratibu kampeni dhidi ya uovu unaofanywa na serikali. MRADI WA...
Mwana-Habari Menna Alaa Ashambuliwa na Wafuasi wa Morsi
Mwanablogu na mwanahabari wa video Menna Alaa leo hii ameshambuliwa na waandamanaji wenye hasira wanaomwunga mkono Morsi. Mwanablogu huyo ameweka ushuhuda wake kwa lugha ya kiingereza kwenye makala hii iliyo katika blogu inayokusanya matukio nchini Misri iitwayo Egyptian Chronicles. Anaandika: Kofi nililopigwa usoni, alama iliyobaki usoni mwangu pamoja na kuibwa...
Wanawake Watatu Wauawa katika Maandamano ya Kumtetea Morsi
Waandamanaji wanaomuunga mkono Morsi wameshambuliwa na mahuni huko Mansoura, tukio lililopelekea wanawake wasiopungua watatu kuuawa pamoja na makumi mawili wengine kujeruhiwa. Watumiaji wa mtandao wameonesha hisia zao kufuatia shambulio hilo.
Shindano la Wanablogu wa Kiafrika wenye Fikra Pevu.
Mtandao wa Africa Brains watangaza Shindano la Wanablogu wa Kiafrika Wenye Fikra Pevu watakaowania kitita cha dola Hamsini ($50). Ni muda muafaka wa kutangaza mada ya kwanza, ambayo ni “Teknolojia imekuwa na ushawishi gani katika elimu yako?” Tufahamishe hali ya upatikanaji wa teknolojia ulipokuwa shuleni au chuoni? Tangu uanze kutumia...
India: Chakula Chenye Sumu Chaua Watoto 24
Chakula kilichoua wanafunnzi na kuwaacha wengine katika hali mbaya kinasadikiwa kuwa kilichanganyikana na dawa ya kuulia wadudu. Tukio hili linaibua maswali kuhusiana na ubora wa chakula cha mchana wanachopewa wanafunzi wanaotoka katika familia masikini.
Maandamano Yasitisha Ujenzi wa Mtambo wa Nyuklia Kusini mwa China
Kufuatia siku tatu mfululizo za maandamano, inaonekana kuwa serikali ya Manispaa ya Heshan katika jiji la Jiangmen imesitisha mpango wake wa ujenzi wa mtambo mkubwa wa nishati ya Nyuklia. Baadhi ya watu wanaamini kuwa ushindi huu ni wa muda mfupi tu. Wana wasiwasi kuwa, mradi huu unaweza kuibukia sehemu nyingine karibu na Delta ya mto Pearl, Kusini mwa China mahali palipo na idadi kubwa sana ya watu.
Hali ya Kidiplomasia Kati ya Zimbabwe na Nchi za Magharibi
Simukai Tinhu, mchambuzi wa masuala ya siasa anayeishi London, anauliza, “Je, mahusiano ya Zimbabwe na nchi za kimagharibi yanaimarika kadri uchaguzi unavyokaribia?”
Wakazi wa Jiangmen Nchini China Wapinga Ujenzi wa Mtambo wa Uranium
Siku ya tarehe 12 Julai, 2013, mamia kadhaa ya wakazi wa Jiangmen, jiji lililo jirani na Guangzhou ya Kusini nchini China, walifurika mtaani na kuandamana kupinga mpango wa kuanzisha mtambo wa kuchakata Urani.