Habari kuhusu Kiingereza kutoka Disemba, 2012
Habari za Upotoshaji Kuhusu Afrika Katika Vyombo vya Habari vya Kimataifa
Kampeni ya kumkamata #Kony2012 ilibeba mambo yaliyorahisishwa mno kuhusu Afrika. Vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe, hata hivyo, kwa sasa havina kinga dhidi ya ukosoaji wa aina hii. Hapa ni muhtasari wa watu maarufu, makosa na kutokuwepo umakini katika habari zinazopewa nafasi katika vyombo vya habari vya dunia kuhusu Afrika na katika vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe
Kitabu-pepe Kipya cha GV: Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko
"Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko", kinakupa mtazamano wa kipekee kuhusu watu na habari za eneo la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia posti zetu zilizo bora zilizoandikwa kwa lugha ya Kiingereza kwa mwaka 2012. Hii ni zawadi sahihi kabisa ya kuukaribisha mwaka mpya.
Video ya Kuomba Ujenzi wa Vyoo vya Umma huko Jharkhand, India
Amit Topno, mwakilishi wa jumuiya ya hiari “inayopiga picha za video” aliripoti kwamba wakati wa kijiji cha Nichitpur katika Jimbo la Jharkhand hawana choo chochote cha umma kinachotumika. Wanavijiji wanaziomba mamlaka za serikali za mitaa kupitia video hii kuhakikisha kuwa vyoo vinavyostahili matumizi ya binadamu vinajengwa.
Chama cha Upinzani NPP Chapinga Matokeo ya Urais Ghana Mahakamani
Chama Kikuu cha Upinzani nchini Ghana, NPP, kimegoma kuyakubali matokeo ya uchaguzi wa Rais. Mnamo tarehe 9 Desemba 2012, Tume ya Uchaguzi ilimtangaza Rais Mahama kuwa mshindi kwa asilimia 50.70 ya kura, akimshinda mshindani wake wa maribu Nana Akufo-Addo wa NPP. Chama cha NPP hapo awali kilifungua mashitaka katika Mahakama Kuu tarehe 28 Desemba, 2012.
China Inaelekea Wapi kwa Mwaka 2013?
Kadri mwaka wa 2012 unavyosogea karibu, jarida la CHINA DIGITAL TIMES limetoa muhtasari wa mabadiliko na changamoto zinazoikabili China mwaka 2013 kwa kutumia taarifa na bashiri mbalimbali za vyombo vya habari.
Assad atumia Ndege ya Kivita Kuwaua Raia Wake
Serikali ya Syria imefanya shambulizi kubwa la angani dhidi ya raia wa nchi hiyo -waliokuwa wamesimama kwenye foleni waisubiri mikate kwenye kiwanda cha kuokea miakte huko Halfaya, Hama. Inakadiriwa kwamba watu waliouawa katika shambulio hilo mjini humo ni kati ya 90 na 300, waasi wakisema kuwa watu hao walikuwa wamejitenga na vikosi vya Assad. Mtandaoni, wanaharakati wanashangazwa inakuwaje dunia inaendelea kutazama tu maisha ya watu wasio na hatia wakiuawa kwa mamia.
Maisha Binafsi ya Watawala Wapya wa China
Shirika la Habari la Xinhua lilichapisha[zh] mfululizo wa wasifu wa maisha binafsi ya watawala wa juu China, ikiwa ni pamoja na picha za familia zao, ambazo ni nadra sana katika vyombo vya habari vya China. Hatua hiyo imechukuliwa na wengi kama dalili nyingine kuwa utawala mpya wa China unaweza ukawa...
Kupigia Kura Maajabu Saba ya Dunia barani Afrika
Shindano la kila mwaka limezinduliwa kwa ajili ya watu kupiga kura kuchagua maajabu saba yaliyo bora zaidi barani Afrika. Na tayari upigaji kura umeshaanza. Baadhi ya maajabu ya asili yaliondolewa katika orodha ya mwisho ya kupigiwa kura na hivyo baadhi ya wanablogu waliongeza mapendekezo yao katika blogu zao. Tazama baadhi ya picha hapa:
Korea Kusini: Mpango wa Kuwakutanisha Wenzi Wakwama
Mpango mpya kabisa wa kuwakutanisha wenzi kwa njia rahisi katika mkesha wa Krismas nchini Korea Kusini hatimaye ulijikuta ukishindwa kabisa baada ya waliojitokeza asilimia 90 kuwa ni wanaume. Inasemekana zaidi ya watu 20,000 walijiandikisha na hata polisi walikuwepo kufuatia uwezekano wa vitendo vya ngono za kulazimisha. Mtumiaji mmoja wa mtandaoalibainisha [ko]...
Ni Sikukuu ya Kuzaliwa Kristo (Noeli) Mjini Betlehemu
Ni sikukuu ya kuzaliwa Kristo mjini Betlehemu, katika ukanda wa Magharibi, Palestina, mahali alipozaliwa Yesu Kristo. Ni namna gani nzuri ya kusherehekea tukio hili zaidi ya kuwashirikisha picha na maoni mbalimbali ya watumiaji wa mtandao wa intaneti kuhusiana na tukio hili linalosherehekewa na mabilioni ya watu duniani kote.